Wednesday, December 16, 2015

SOMO: KIJANA NA UCHUMI.


Bwana Yesu asifiwe wapendwa, Natumai mu wazima tena. We thank God for this precious day, na leo ntaenda kufundisha somo juu ya kijana na uchumi.
Kwanza inawezekana haujui au bado hujatambua kwamba kijana ni wa thamani sana mbele za Mungu. sisemi kwamba wengine sio wa thamani au hawana umuhimu kwa Mungu, hapana! nimesema hivyo kwa sababu kuna mambo ambayo yanamfanya kijana kuwa wa muhimu sana
1 kijana ni mwenye nguvu(Mithali 20:29, 1Yoh 1:14)
2 ni wakati wa kujenga foundation/msingi wa maisha(future yako)
3 ni wakati sahihi wa kumtumkia Mungu(Muhubiri 12)
Sasa hizo ni baadhi ya sababu za kujua kwanini wewe ni muhimu sana na shetani anajua hilo pia ndio maana wakati wa ujana huna shida sana maana shetani ana deal sana na vijana.
Nisiendelee sana huko maana hilo pia ni somo lingine kati ya masomo nilionayo, ila tuangalie hili la leo''KIJANA NA UCHUMI''
Vijana wengi tumekua tukipata shida katika eneo la uchumi na mwisho wa siku tunajikuta hatuna kitu kabisa. japo kuna maroho ya umaskini na ufukara yanayo fuatilia watu wa Mungu, lakini zipo circumstance ambazo tunajisababishia sisi wenyewe.
Kuna matatizo yanayowapata wengi hasa katika eneo hili la uchumi mwisho wa siku unajikuta mambo mengi hayaendi na unakata tamaa na kuhisi huna bahati. Wapo wanaoshindwa kuoa, kujikimu ndani ya familia zao, kupata maitaji yao ya kila siku, tatizo kubwa likiwa uchumi mbovu.
Labda tuanze na'' KWANINI MTU ANAPATA PESA LAKINI HAIKAI?
Zipo sababu ambazo hupelekea haya na hili tatizo limetukumba wengi sana, mimi nikiwa mmoja wapo ila namshukuru Mungu alienifunulia haya na ndio maana nakushirikisha ili tujikomboe na wote kufurahia matunda ya pesa zetu
Sababu ya kwanza
1 KUTOKUMUHESHIMU MUNGU KWA MALI NA FEDHA
Mithali 3:9-10 anasema mheshimu Bwana kwa mali yako na kwa malimbuko na mazao yako yote, ndipo ghala zako zitakapo jazwa kwa wingi. Wapendwa embu tafakari hayo maneno hapo, yaani unapomheshimu Mungu kwa mali yeye anakujazi ndio maana yake.
Mathayo 6:19-21, Hagai 1:2-8 Katika maandiko haya swaa zima hapa ni utoaji nikimaanisha sadaka,michango kanisani n.k Mathayo anasema usijiwekee hazina Duniani, kwaiyo tunaona Mungu anataka na anaheshimu unapo mtumikia kwa mali na fedha. ukiangali hiyohiyo mstari wa 31 anasema utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na hayo mengine mtazidishiwa.
Malaki 3:8-10 hapa anaongelea zaka tena kamili sio nusu maana kuna watu wanatoa ndio ila sio kamili, ndugu bora usitoe maana ambaye ajatoa na wewe wa nusu ni sawa tu kumbuka anania na saphira( Mdo 5).
2 KUTAMANI KUISHI MAISHA YANAYOKUZIDI UWEZO
Wapo watu wanaotamani kuishi wakati hali yao ya uchumi hairusu.Labda siku Mungu kakubariki ila tatizo linakuja pale flani au rafiki yako ana simu ya samsung note gear basi na wewe unataka hiyo gear wakati hali ya mfuko wako ni techno mchina...utajikuta unatumia fedha ambazo hukupangilia kununua simu ya gharama kubwa, ndugu ridhika na ulichonacho. Waebrania 13:5 anasema msiwe na tabia ya kupenda fedha muwe radhi na mlivyo nayo. 1Tim 6:6 anasema walakini utauwa pamoja nakuridhika ni faida kubwa.
3 MATUMIZI BILA MALENGO/MIPANGO
Hapa napo panashida sana tu. Wengi hatutumii pesa kwa malengo au mipango. Ndugu unatakiwa kuwa na mipango kwa mfano unaweza ukawa unamuomba mtu pesa kila siku alafu jibu lake ni sina......sio kwamba kila siku yeye hana, hapana! zipo ila zimepangiliwa kwaiyo ya kukupa wewe haipo.Unaweza ukakuta umepokea mshahara..mzuri tu ila kama ujapangilia unaweza ukaisha siku hiyohiyo kwa vijisababu visivyo eleweka mara baby kaja anataka hiki na kile mara mmeenda kula bata mara mmeamua kubadilisha mazingira hata nyumbani hapalaliki siku hiyo...mwingine kwa sababu kapata mshahara atataka watu wajue basi oa zitatembea siku balaaa! alafu mtu akiishiwa anaomba maombi kwa pastor!!!! kua ana pepo la umaskini linamfuatilia kumbe ni kutofahamu.
4 KUMDHULUMU MUNGU
Kumb 16:17 anasema kila mtu na atoe kama Mungu atakavyombariki. kumbuka yule mama mjane alitoa kidogo sana maana ndicho alichokua nacho ila angalia Yesu alivyosema.Je utoavyo sadaka kanisani, michango yako ya ujenzi,injili, mafungu ya kumi, ni kama unavyobarikiwa? jibu unalo moyoni. Mdo 5
Kwaiyo labda kabla ya deliverance na maombezi jichunguze kwanza je katika sababu hizi nilizotaja zinakuhusu na kama zinakuhusu anza leo kujirekebisha na kama bado kuna shida, basi hapo ndio tuanze na maombi maana kama nilivyosema hapo juu kuna maroho ya ufukara na umaskini yanayofuatilia watu.
Mungu na atusaidie sote....STAY INSPIRED!!!

9 comments: