Saturday, December 12, 2015

SOMO: UTAKATIFU NDIO MSINGI WA MAISHA YA MKRISTO.


Bwana Yesu Asifiwe, Namshukuru Mungu kwa nafasi nyingine tena. Napenda kukushikisha tena katika moja ya masomo yangu, kama linavyosomeka hapo juu.
UTANGULIZI
Wengi tunadhani kuwa mtu ukishaokoka ni raha tuu na starehe hadi pale yesu atakapo kuja kuchukua kanisa lake. Waebrania 12:14"tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu ambao hapana mtu atakayemwona bwana asipokuwa nao" Kwenda mbinguni ni process yenye stages;
1 KUOKOKA
2KUISHI MAISHA MATAKATIFU, kuokoka peke yake hakutoshi kwa wewe kwenda mbinguni.
Msingi ni nini? kamusi inasema, msingi ni kitako cha nyumba, ambapo nyumba hujengwa au kitu cha mwanzo ambacho ni muhimu kuwepo kabla ya vitu vingine kujengwa juu yake au jambo muhimu. kwaiyo baada ya kuona hiyo maana ya msingi tunaweza tukasema, utakatifu ni jambo muhimu kwa mkristo, Mambo ya walawi 11:44" kwa kuwa mimi ni Bwana wenu takaseni nafsi zenu, basi iweni watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu"
Tuanze kwa kuangalia maandiko machache, Mathayo 7:24-25" basi kila asikiaye hayo maneno yangu, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba. mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma zikaipiga nyumba ile isianguke kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba" Tunaona kwamba mkristo anaye ishi maisha matakatifu ana fananishwa na nymba iliyojengwa juu ya mwamba, pata picha umejenga nyumba bila ya msingi alafu mafuriko siku yakaja unafikiri nini kitatokea???? kwaiyo wewe ni nyumba na kama ukiishi maisha ya utakatifu basi umeijenga misingi yako juu ya mwamba.
Mithali 10:25" kisulisuli kikiisha pita asiye na haki hayuko tena, bali mwenye haki ni msingi wa milele. tunaendelea kuona kwamba hata misukosuko yaani majaribu na kama Biblia inavyosema majaribu hayanabudi kuja kwaiyo pamoja na hayo yote mwenye haki atayashinda maana ana msingi wa milele ambao ni utakatifu. ukianglia Zaburi 1:6 anaendelea kusisitiza "kwa kuwa bwana anaijua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea"
1 Wakorinto 3:11" maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka isipokuwanni ule uliokwisha kuwekwa, yaani yesu kristo" Hapa tunaona kuwa yesu kristo ndio msingi wa maisha yetu. tukiisha kumpokea kama bwana na mwokozi wa maisha yetu hatuishii hapo na ndio maana paulo anasema tuenende kama inavyoipasa injili ya kristo maana yake tuishi kama yeye( YESU). pia ukiangalia Mithali 16:17 anasema "njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu"
Unajua mara nyingi tunaanguka majaribuni, hatufanikiwi, kwasababu tunaishi maisha ya kuigiza. unakuta mtu ameokoka ila uwezi kumtofautisha na ambae hajaokoka. nilikutana na rafiki yangu ambae nilipomshuudia habari za yesu alikubali ila kuna kitu aliniambia nami nilimpenda sana kwa kuwa mkweli.......alisema anapenda sana kuokoka ila nimpe mda afikirie na afanye maamuzi ya busara ili kama ataamua na aamue moja kwa moja. sio siri yaani yule jamaa alinifurahisha sana na nina hakika kama ataokoka siku basi atatushinda hata sisi tuliotangulia ambao tunasuasua. Biblia inasema ni heri kuwa moto au baridi ila sio vuguvugu.
i argue you brothers....lets live a holy life as its a foundation to our everyday life.

7 comments:

  1. very true pastor be blessed

    ReplyDelete
  2. Ujumbe ni mzuri sana kwamaana utakatifu ndio msingi wa wokovu.

    ReplyDelete
  3. Barikiwa Sana maana hatuweziurithi ufalme wa Mungu bila utakatifu na mtakatifu ni mtu aliyetengwa kwa kusudi la Mungu na kusudi la Mungu ni kutupa uzima wa milele

    ReplyDelete
  4. Mungu akubalik San

    ReplyDelete
  5. Mungu akubariki mchungaji kwa solo lako

    ReplyDelete