Friday, November 27, 2015

SOMO: UNAITUMIAJE NEEMA ULIONAYO?

Bwana yesu asifiwe friends, ni matumaini yangu mu wazima wa afya. ni siku nyingine tena ambayo bwana ametuwezesha kuiona. napenda kukushirikisha somo jingine ambalo bwana amenipa.
UTANGULIZI:
Kwanza tuanze kwa kuangalia neema ni nini? katika tafsiri ya kamusi ya kisasa inasema, neema ni mafanikio alionayo mtu kutokana na majaliwa ya mwenyezi mungu au juhudi zake, baraka n.k. kwa tafsiri yangu, Neema ni nafasi ya upendeleo au kuchaguliwa bila kustahili.
Wengi tunafikiri kuwa imetoketokea tu tupo hai hadi sasa hivi, si mgonjwa, si kilema, huna matatizo alafu unajisifu ukidhani wewe unafaa sana mbele za Mungu. kama tulivyoona hapo juu, umependelewa au umechaguliwa bila kustahili.
Hivi fikiria kwa mfano leo Mungu akakutokea alafu aseme anataka kukuchukua pumzi yake au la umpe mabilioni ya pesa!!!! nani angeweza?????.....kwaiyo bado ukijaribu kutafakari unaona kwamba umepewa nafasi(CHANCE) bila kustahili.
ukisoma yakobo 4:6 inasema'' mungu huwapinga wajikuzao bali huwapa neema wanyenyekevu.
waefeso 2:8-9, paulo anasema''kwa maana nimeokolewa kwa neema kwa njia ya imani ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu ni kipawa cha Mungu wala si kwa matendo mtu yeyote asije akajisifu.....heri yake paulo alijua kwamba kuishi kwetu ni neema yake mungu...Wapo watu wanaojisifu. jamani tambueni kuwa umepewa neema na Mungu wala si kwa mapenzi yako ila ni kwa makusudi yake...Nimetoa mfano hapo juu, kwamba kama Mungu angesema tumlipe kwa pumzi yuliyonayo, basi dunia ingekua haina mtu.2wakorinto 1:12, 6:1''Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure....
SASA UNAITUMIAJE NEEMA ULIYONAYO?
tuangalie tena 1Wakorinto 15:10''Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyokuwa kwangu si bure bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote wala si mimi bali ni neema ya Mungu pamoja nami.... Hapa tunaona paulo anasema kwa sababu hivo alivyo ni kwa neema ya mungu basi alizidi sana kufanya kazi kupita wote. Kwaiyo baada ya kutambua kuwa umepewa neema, ni vyema sasa ukaishi katika mapenzi yake kwelikweli maana mda wowote atataka umrudishie pumzi yake.
2Timotheo 2:1''Basi wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu...Anaposema tuwe hodari maana yake ni tufanye kazi ya mungu kwelikweli hali tukijua kuwa neema tuliyonayo hatukustahili. Pia kuitumia vizuri neema yetu ni kuzidi kutenda mema na kuwa watakatifu maishani mwetu.(SISI NI WASAFIRI DUNIANI)
somo hili mungu alinipa kwa makusudi yake na ni naamini kuwa wakristo tuliowengi bado hatujajua kuwa tunaishi kwa neema na neema hiyo tumepewa kwa kusudi lake....Kuna wengine tunaishi maisha ya uvugu uvugu, hatutaki kuwa committed na kazi ya Bwana. Endelea tu kufanya dhambi, maana hata biblia inasema mwenye dhambi na azidi kufanya dhambi na mtakatifu na azidi kujitakasa...sasa wewe utajua ufanyeje maana mtu mzima alazimishwi ila anachuja kabla ajafanja.ni ombi langu kuwa kuanzia leo, ebu tuanze kuitumia neema hii ipasavyo, Mungu anatuangalia tu na kutupima,kuna siku atachukua neema yake na ndipo utajuta kuwa kwa nini uliichezea...soma zaburi103:8-9 anasema''bwana amejaa huruma na neema, haoni huruma upesi, ni mwingi wa fadhili. Kwaiyo Mungu anatuvumilia tu ila ataposema sasa yatosha, Ndugu hakika utajuta.pia ukisoma warumi 2:4-5 inasema'' au waudharau wingi wa wema wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta uapate kutubu... mstari wa tano unasema kwa ugumu wa moyo wako wajiwekea hakiba ya hasira ya mungu katika siku ile ya hukumu.
kwaiyo Ndugu zangu tutumie hii neema vizuri ingali tuliwa hai....
MUNGU AWABARIKI SANAAA!!!!!!
unaweza kunipata pia katika facebook kwa mafundisho zaidi.
shalom!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment