Saturday, December 26, 2015

SOMO: TUVUE MIILI YETU, TUKAMVAE YESU.

SHALOM!! Namshukuru Mungu sana sana kwa wingi wa fadhili na neema zake kwetu, hakuna mtu ambae alistahili kuiona siku ya leo. juzi nilikua naangalia taarifa kuna jamaa kakatwa mapanga na kufa palepale, jiulize we ni nani au umempa Mungu nini kwa uhai ulionao? kristmas imepita tunatazamia kuuona mwaka mpya..ambayo ni wiki ijayo tu ila tuendelee kumsihi Mungu atuvushe kwa ushindi.
Leo ntawashirikisha somo kama linavyosomeka hapo juu.....inawezekana ukajiuliza huyu Yesu tunamvaaje? Wengi wetu tuna lundo la nguo ambazo tunavaa na kubadilisha kila siku hakuna anae penda kuvaa nguo ileile siku zote hata kama hana ila anatamani siku awenazo nyingi. sasa ninaposema tuvue miili yetu na tumvae Yesu namaanisha kuacha mambo yakale na kuishi maisha mapya. Nimetoa mfano wa nguo maana ni kitu ambagho kinavaliwa kila siku ila sasa tofauti inakuja kwamba tukishamvaa Yesu, yeye anakua ni vazi la kudumu tofauti na nguo za kawaida hakuna haja ya kuvumvua tena.
Tuangalie katika Waefeso 4:22-24 anasema " Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu ktk haki na utakatifu wa kweli. maandiko tuliyosoma hapo juu yako wazi sana. kwaiyo tunapofanywa upya, tunapotubu na kuishi maisha matakatifu, tunapookoka ina maana tunavua miili yetu na kumvaa Yesu. wengi wetu leo bado wanang'ang'ania miili yao ya zamani wakati washampokea Yesu kristo. ndugu ni ngumu kushinda dhambi kama tunaishi katika mwili. sasa tumapo mva Yesu ni rahisi sana maana yeye ndo anatushindia yote.
Rum 8:13 inasema "kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. kwaiyo bado tunazidi kuona kwamba miili yetu haiwezi kustahimili dhambi bali tuyafisha mambo ya mwili kwa Roho ambayo ndo sawa na kusema kumvaa Yesu hakika tutaweza.
Pia tukiangalia katika Wagalatia 5:16 inasema" basi enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. neno hapa linasema mwili hunashindana na Roho, kumbuka Yesu alisema katika mathayo kwamba Roho i radhi ila mwili u dhaifu......kwaiyo kwa kumvaa Yesu na kuvua miili yetu ndo kuenenda pamoja na Roho ambae ndo anatusaidia kuweza. sura ya 6:8 anasema " maana yeye apandaye kwa mwili atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. 3:27 inasema "maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo, mmemvaa Kristo. pia Paulo anasema sura ya 2:20 " nimesulubiwa pamoja na Kristo,laakini ni hai, wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu.
Paulo anaendelea katika wafilipi 1:21 anasema" kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Kwaiyo wapenzi katika somo hili tunaona kuwa tukiishi katika miili hii pasipo msaada wa Roho ni vigumu kumpendeza Mungu, na huo msaada wa roho unakujaje ni pale tunapo mvaa Yesu kama maandiko yanavyosema
.
Tukiwa tunaelekea mwaka mpya, ni maombi yangu kuwa tuanze sasa na Bwana, tusahau yaliopita ya mwaka 2015.....anasema katika neno lake ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya. kama tumvaa yesu kikwelikweli hakika mwaka 2016 kwako unaenda kuwa wa mafanikio na baraka tele, yale ulioomba mda mrefu yatatimia kwa jna la Yesu!!!!!
Anza 2016 na maisha mapya na hakika utamwona Bwana..........................................
STAY INSIPIRED!!!!!!!!!!!!!!!

Wednesday, December 16, 2015

SOMO: KIJANA NA UCHUMI.


Bwana Yesu asifiwe wapendwa, Natumai mu wazima tena. We thank God for this precious day, na leo ntaenda kufundisha somo juu ya kijana na uchumi.
Kwanza inawezekana haujui au bado hujatambua kwamba kijana ni wa thamani sana mbele za Mungu. sisemi kwamba wengine sio wa thamani au hawana umuhimu kwa Mungu, hapana! nimesema hivyo kwa sababu kuna mambo ambayo yanamfanya kijana kuwa wa muhimu sana
1 kijana ni mwenye nguvu(Mithali 20:29, 1Yoh 1:14)
2 ni wakati wa kujenga foundation/msingi wa maisha(future yako)
3 ni wakati sahihi wa kumtumkia Mungu(Muhubiri 12)
Sasa hizo ni baadhi ya sababu za kujua kwanini wewe ni muhimu sana na shetani anajua hilo pia ndio maana wakati wa ujana huna shida sana maana shetani ana deal sana na vijana.
Nisiendelee sana huko maana hilo pia ni somo lingine kati ya masomo nilionayo, ila tuangalie hili la leo''KIJANA NA UCHUMI''
Vijana wengi tumekua tukipata shida katika eneo la uchumi na mwisho wa siku tunajikuta hatuna kitu kabisa. japo kuna maroho ya umaskini na ufukara yanayo fuatilia watu wa Mungu, lakini zipo circumstance ambazo tunajisababishia sisi wenyewe.
Kuna matatizo yanayowapata wengi hasa katika eneo hili la uchumi mwisho wa siku unajikuta mambo mengi hayaendi na unakata tamaa na kuhisi huna bahati. Wapo wanaoshindwa kuoa, kujikimu ndani ya familia zao, kupata maitaji yao ya kila siku, tatizo kubwa likiwa uchumi mbovu.
Labda tuanze na'' KWANINI MTU ANAPATA PESA LAKINI HAIKAI?
Zipo sababu ambazo hupelekea haya na hili tatizo limetukumba wengi sana, mimi nikiwa mmoja wapo ila namshukuru Mungu alienifunulia haya na ndio maana nakushirikisha ili tujikomboe na wote kufurahia matunda ya pesa zetu
Sababu ya kwanza
1 KUTOKUMUHESHIMU MUNGU KWA MALI NA FEDHA
Mithali 3:9-10 anasema mheshimu Bwana kwa mali yako na kwa malimbuko na mazao yako yote, ndipo ghala zako zitakapo jazwa kwa wingi. Wapendwa embu tafakari hayo maneno hapo, yaani unapomheshimu Mungu kwa mali yeye anakujazi ndio maana yake.
Mathayo 6:19-21, Hagai 1:2-8 Katika maandiko haya swaa zima hapa ni utoaji nikimaanisha sadaka,michango kanisani n.k Mathayo anasema usijiwekee hazina Duniani, kwaiyo tunaona Mungu anataka na anaheshimu unapo mtumikia kwa mali na fedha. ukiangali hiyohiyo mstari wa 31 anasema utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na hayo mengine mtazidishiwa.
Malaki 3:8-10 hapa anaongelea zaka tena kamili sio nusu maana kuna watu wanatoa ndio ila sio kamili, ndugu bora usitoe maana ambaye ajatoa na wewe wa nusu ni sawa tu kumbuka anania na saphira( Mdo 5).
2 KUTAMANI KUISHI MAISHA YANAYOKUZIDI UWEZO
Wapo watu wanaotamani kuishi wakati hali yao ya uchumi hairusu.Labda siku Mungu kakubariki ila tatizo linakuja pale flani au rafiki yako ana simu ya samsung note gear basi na wewe unataka hiyo gear wakati hali ya mfuko wako ni techno mchina...utajikuta unatumia fedha ambazo hukupangilia kununua simu ya gharama kubwa, ndugu ridhika na ulichonacho. Waebrania 13:5 anasema msiwe na tabia ya kupenda fedha muwe radhi na mlivyo nayo. 1Tim 6:6 anasema walakini utauwa pamoja nakuridhika ni faida kubwa.
3 MATUMIZI BILA MALENGO/MIPANGO
Hapa napo panashida sana tu. Wengi hatutumii pesa kwa malengo au mipango. Ndugu unatakiwa kuwa na mipango kwa mfano unaweza ukawa unamuomba mtu pesa kila siku alafu jibu lake ni sina......sio kwamba kila siku yeye hana, hapana! zipo ila zimepangiliwa kwaiyo ya kukupa wewe haipo.Unaweza ukakuta umepokea mshahara..mzuri tu ila kama ujapangilia unaweza ukaisha siku hiyohiyo kwa vijisababu visivyo eleweka mara baby kaja anataka hiki na kile mara mmeenda kula bata mara mmeamua kubadilisha mazingira hata nyumbani hapalaliki siku hiyo...mwingine kwa sababu kapata mshahara atataka watu wajue basi oa zitatembea siku balaaa! alafu mtu akiishiwa anaomba maombi kwa pastor!!!! kua ana pepo la umaskini linamfuatilia kumbe ni kutofahamu.
4 KUMDHULUMU MUNGU
Kumb 16:17 anasema kila mtu na atoe kama Mungu atakavyombariki. kumbuka yule mama mjane alitoa kidogo sana maana ndicho alichokua nacho ila angalia Yesu alivyosema.Je utoavyo sadaka kanisani, michango yako ya ujenzi,injili, mafungu ya kumi, ni kama unavyobarikiwa? jibu unalo moyoni. Mdo 5
Kwaiyo labda kabla ya deliverance na maombezi jichunguze kwanza je katika sababu hizi nilizotaja zinakuhusu na kama zinakuhusu anza leo kujirekebisha na kama bado kuna shida, basi hapo ndio tuanze na maombi maana kama nilivyosema hapo juu kuna maroho ya ufukara na umaskini yanayofuatilia watu.
Mungu na atusaidie sote....STAY INSPIRED!!!

Saturday, December 12, 2015

SOMO: UTAKATIFU NDIO MSINGI WA MAISHA YA MKRISTO.


Bwana Yesu Asifiwe, Namshukuru Mungu kwa nafasi nyingine tena. Napenda kukushikisha tena katika moja ya masomo yangu, kama linavyosomeka hapo juu.
UTANGULIZI
Wengi tunadhani kuwa mtu ukishaokoka ni raha tuu na starehe hadi pale yesu atakapo kuja kuchukua kanisa lake. Waebrania 12:14"tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu ambao hapana mtu atakayemwona bwana asipokuwa nao" Kwenda mbinguni ni process yenye stages;
1 KUOKOKA
2KUISHI MAISHA MATAKATIFU, kuokoka peke yake hakutoshi kwa wewe kwenda mbinguni.
Msingi ni nini? kamusi inasema, msingi ni kitako cha nyumba, ambapo nyumba hujengwa au kitu cha mwanzo ambacho ni muhimu kuwepo kabla ya vitu vingine kujengwa juu yake au jambo muhimu. kwaiyo baada ya kuona hiyo maana ya msingi tunaweza tukasema, utakatifu ni jambo muhimu kwa mkristo, Mambo ya walawi 11:44" kwa kuwa mimi ni Bwana wenu takaseni nafsi zenu, basi iweni watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu"
Tuanze kwa kuangalia maandiko machache, Mathayo 7:24-25" basi kila asikiaye hayo maneno yangu, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba. mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma zikaipiga nyumba ile isianguke kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba" Tunaona kwamba mkristo anaye ishi maisha matakatifu ana fananishwa na nymba iliyojengwa juu ya mwamba, pata picha umejenga nyumba bila ya msingi alafu mafuriko siku yakaja unafikiri nini kitatokea???? kwaiyo wewe ni nyumba na kama ukiishi maisha ya utakatifu basi umeijenga misingi yako juu ya mwamba.
Mithali 10:25" kisulisuli kikiisha pita asiye na haki hayuko tena, bali mwenye haki ni msingi wa milele. tunaendelea kuona kwamba hata misukosuko yaani majaribu na kama Biblia inavyosema majaribu hayanabudi kuja kwaiyo pamoja na hayo yote mwenye haki atayashinda maana ana msingi wa milele ambao ni utakatifu. ukianglia Zaburi 1:6 anaendelea kusisitiza "kwa kuwa bwana anaijua njia ya wenye haki, bali njia ya wasio haki itapotea"
1 Wakorinto 3:11" maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka isipokuwanni ule uliokwisha kuwekwa, yaani yesu kristo" Hapa tunaona kuwa yesu kristo ndio msingi wa maisha yetu. tukiisha kumpokea kama bwana na mwokozi wa maisha yetu hatuishii hapo na ndio maana paulo anasema tuenende kama inavyoipasa injili ya kristo maana yake tuishi kama yeye( YESU). pia ukiangalia Mithali 16:17 anasema "njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu"
Unajua mara nyingi tunaanguka majaribuni, hatufanikiwi, kwasababu tunaishi maisha ya kuigiza. unakuta mtu ameokoka ila uwezi kumtofautisha na ambae hajaokoka. nilikutana na rafiki yangu ambae nilipomshuudia habari za yesu alikubali ila kuna kitu aliniambia nami nilimpenda sana kwa kuwa mkweli.......alisema anapenda sana kuokoka ila nimpe mda afikirie na afanye maamuzi ya busara ili kama ataamua na aamue moja kwa moja. sio siri yaani yule jamaa alinifurahisha sana na nina hakika kama ataokoka siku basi atatushinda hata sisi tuliotangulia ambao tunasuasua. Biblia inasema ni heri kuwa moto au baridi ila sio vuguvugu.
i argue you brothers....lets live a holy life as its a foundation to our everyday life.

Monday, December 7, 2015

SOMO: UMEPEWA NEEMA ILI UPATE KUTUBU.


Bwana yesu asifiwe, namshukuru sana Mungu kwa matendo yake siku hadi siku, na kwa kuwapa uzima had kuifikia siku ya leo tena.
Ni wakati mwingine katika mwendelezo wa masomo yangu, kama linavyosomeka hapo juu. umepewa neema ili upate kutubu.
Wengi hatutambui umuhimu wa neema tulionayo maishani mwetu, kwanza tuanzae kwa kuangalia nini maana ya toba.
Toba ni badiliko la nia akilini, ambayo matokeo yake yamo katika matendo yaliobadilika kwenye kamusi anasema{ majuto kutokana na maovu uliofanya}. Watu wengi wanafananisha msamaha na toba, ingawa vinauhusiano kwa karibu sana. Msamaha ni tendo la kuomba radhi kwa kosa...... sasa kwa mfano mtu akitaka kuokoka anaongozwa sala ya toba....maana yake ukishaongozwa sala ya toba alafu hakuna badiliko katika maisha yako, hiyo siyo toba ya kweli....
Matendo 26:20" bali kwanza niliwahubiri wale wa dameski na yerusalemu na katika nci yote ya uyahudi, na watu wa mataifa kwamba watubu na kumwelekea Mungu, wakitenda matendo yanayopatana na kutubu kwao"
Tuangalie Luka 3:8" basi toenii matunda yapasayo toba" matunda yapasayo toba maana yake kubadilika. tumeona hapo juu kuwa toba ni badiliko kwaiyo nia ya somo hili ni kwamba wengi wetu ni wakristo, tulishaongozwa sala ya toba ila sasa bado hatuzai matunda yapasayo toba kama luka inavyosema. sasa Mungu ametupa neema ya kuishi, tuliona katika somo la UNAITUMIAJE NEEMA ULIONAYO, ila hatujajua kama hiyo neema tuliopewa ni ili tutubu au tuishi matunda yapasayo toba.
Warumi 2:4-5" au waidharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue wema wa Mungu wakuvuta ili uape kutubu" kwaiyo tunazidi kuona kwamba Mungu anatuvumilia au neema yake bado ipo kwetu ili tuweze kutubu. maana kama nilivyosema katika somo lililopita kwamba , maisha tulionayo tumeazimwa tu, sasa itafika saa Mungu atadai chake. je utakua tayari kumrudishia?
2Petro 3:9" Bwana akawii kutimiza ahadi yake kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee wote waifikilie toba" bado maandiko yako wazi kuwa Mungu kamwe apendi mtu apotee na ndio maana bado neema ipo ili wote sasa tuiifikie ile toba, wapo wanaojisifu juu ya neema walionayo! wewe Bwana acha kabisa........
Wapendwa kuna watu wanaweza kuisi kua ujumbe huu unawahusu ambao wajaokoka! Hapana, maisha tunatoishi hayana tofauti na ambao bado hawajampokea yesu, sasa si hata wao wenyewe si watabaki wanakushangaa tu? maana Biblia inasema utawatambua kwa matendo yao......sasa mpendwa matendo yako hayatokani na kutubu kwako, kwaiyo bila shaka hili somo linakuhusu asilimia mia kabisa.
Ni maombi yangu ifikie kipindi sasa tubadilike na nimekua nikisisitiza sana kwenye masomo yangu maana mda tulio nao ni mchache mno!!!!!! Amani ya Bwana iwe nanyi nyote.....Amina

Sunday, November 29, 2015

SOMO:TUNAMZUIA MUNGU KUTUBARIKI KWA SABABU YA MAOVU YETU.

       Bwana yesu apewe sifa wapenzi wasomaji.........napenda kumshukuru Mungu kwa nafasi alionipa tena, Katika mwendelezo wa masomo yangu, leo nitafundisha juu ya ni kwanini watu wa Mungu wengi hawabarikiwi.
     Kwanza lazima tujue kuwa baraka ni haki yako kabisa kwa sababu ni ahadi ya Mungu mwenyewe, ukisoma kumb 28 utaona jinsi gani ahadi hizo zimetolewa. Sasa mtu unaweza ukajiuliza inakuaje nasema ni haki ya mwamini wakati wewe umekua ni Mtu wa kuwapigia makofi wenzio kanisani wakati  wanashuudia baraka walizopata either Mungu kawasaidia kununua gari, kupata kazi, kujenga nyumba, n.k
        Jibu ni rahisi sana....binafsi namshukuru Mungu kwa sababu amenifunulia siri hii na imekua msaada mkubwa sana katika maisha yangu.
         Wapendwa sisi wenyewe ni chanzo cha kuzuia baraka hizi..........iko hivi, kama kuna kitu ambacho Mungu anapenda kutoka kwetu, basi ni utii wetu kwake(anapenda kuabudiwa, kuheshimiwa). Sasa tatito linaanzia hapa Mtu anataka Mungu ambariki wakati yeye hataki kumtii au kumheshimu. tusome Isaya 59:1-2''tazama mkono wa bwana haukupunguka hata usiweze kukuokoa wala sikio lake sio zito lisiweze kusikia, lakini maovu yenu yamewafarakanisha ninyi na Mungu na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. Jamani haya maandiko nayapenda kwasababu yako wazi sana. yaani ukianzia mstari wa pili anasema, lakini maovu yenu na dhambi zenu zimeuficha uso wake na zimewafarakanisha. kwaiyo tunaona kabisa Mungu ashindwi kukubariki ila dhambi zako ni chukizo mbele zake na ndio kwazo la yeye kukubariki.
     Tusome tene Isaya 1:19'' kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi'' bado anasisitiza kitu   kimoja (UTII). kama nilivyosema hapo juu Mungu ndio kitu anapenda yaani ukimuheshimu ni lazima baraka zitakuja tu.
      Saa nyingine sio lazima hata kuomba, naomba unielewe sisemi kwamba usiombe hapana maombi ni muhimu sana na ndio silaha yetu ila ukijishugulisha na Mungu , yeye anajishugulisha na wewe kwa mfano Mtoto akiwa watii kwa wazazi kiasi cha kumfurahisha, utakuta siku mzazi anampa Mtoto labda zawadi au hela ya matumizi bila hata ya Mtoto yule kuomba. mimi imewahi kunitokea naamini na baadhi yetu pia. 2Nyakati 7:14'' ikiwa Watu wangu walioitwa kwa jina langu watajinyenyekesha na kuomba na kunitafuta uso na kuziacha njia zao mbaya basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi zao na kuiponya nchi''. Haya hapa tuna vitu vitatu, moja ni kijinyenyekesha na kuomba, mbili ni kutafuta uso wa Mungu, tatu ni kuacha njia mbaya. yeye(Mungu) sasa atachofanya, atasikia, atasamehe dhambi na kuponya. Kwaiyo unaitaji nini zaidi maana hapa mstari uko wazi kabisa wajibu wako na wajibu wa Mungu kwako.
      Zaburi 1:1-3 ukiangalia inasema ana heri mtu yule asiekwenda katika shauri la wasio haki, ukisoma biblia ya kiingereza inasema '' BLESSED IS THE MAN'' kwaiyo mtu asieenda katika dhambi amebarikiwa. mstari wa tatu unasema na kila alitendalo litafanikiwa............
     Wapendwa mimi mwenyewe ni shuhuda wa mambo ninayo yasema wala sisemi tu kwa sababu Mungu amenipa somo hili, la hasha! baada ya kupewa somo hili nilijirekebisha pale nilipokosea na  kwa kweli namuona Mungu sana katika Maisha yangu , kuna mambo najikuta yanatokea hadi nashangaa kwasababu hata mengine sikuomba ila nabaki kumshukuru.
    Ndugu mpendwa nawasihi katika Bwana , ifike muda tuache sasa kumlaumu Mungu kwa sababu tatizo ni la kwetu wala si lake. mfano unamkuta mtu analalamika kwenye maombi yake, na ni wazuri sana kwenye kunukuu maandiko utasikia ulisema tutabarikiwa tuingiapo, tutokapo, litabarikiwa kapu langu!!! ungejua unaemlalamikia kwanza hata kukusikia akusikii ungeacha tu.....Kwaiyo ebu tubadikilike sasa tuache maovu na dhambi tunazofanya kwa hakika baraka zitatujilia, maana Mungu si Mwanadamu hata aseme uongo lazima atafanya.

BARIKIWA!!!!!

Saturday, November 28, 2015

SOMO:LAZIMA TUWE NA NENO LA MUNGU ILI TUWEZE KUSHINDA.

        Bwana yesu apewe sifa, Hamjambo na karibuni katika mwendelezo wa masomo yangu.Leo ninalo somo kama linavyosema hapo juu, kwamba ni lazima kuwa na neno la Mungu ili tuweze kushinda.
        Kwanza kabisa neno ni Mungu mwenyewe, soma Yohana 1:1''Hapo mwanzo kulikuwako neno, naye neno alikuwa Mungu. Kwaiyo, tunadhiirishiwa kwamba neno ni Mungu. kwa mantiki hiyo sasa tunaona kuwa kumbe kuwa na neno ni kuwa na mungu mwenyewe.
        Wengi hatujajua kuwa neno ni mungu na kama tunajua sidhani kama wakristo wa sasa tusingependa kusoma neno. Mimi nashangaa sana, yaani sijui mkristo anaishije eti siku inapita hajasoma neno, kwa upande wangu hua najisikia vibaya sanaaaa. Sikatai zipo sababu zinakubana inapita siku hujasoma neno....sawa! ila hakikisha hiyo sababu kweli inakubalika na Mungu na kwa mkristo aliyesimama kweli kweli  lazima aumie ndani au aone utofauti. kama wewe unaona kawaida basi tambua iko shida ndani yako.
       Tuanze kwa kusoma Mathayo 22:29 inasema''Yesu akajibu akawaambia, mwapotea kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa mungu''. Kwaiyo kumbe hawa masadukayo walikua wanapote akwa sababu yakutokujua maandiko. vipi wewe na mimi ambao leo imekua shida kusoma neno la Mungu, alafu bado unataka eti Mungu akuokoe na majaribu yanayokusonga? sikia Yesu alipokuwa akijaribiwa na ibilisi nyikani, alimshinda kwa neno tu...soma Mathayo 4 kuanzia mstari wa kwanza, utaona kila alipokua anajibu alikua ana refer kwenye maandiko. Sasa unaweza ukaona kumbe hata Yesu ambae angeweza na alikua na uwezo wa kumkemea tu shetani na aondoke ila bado nayeye alihitaji neno ili aweze kushinda sembuse mimi na wewe??????
       Ukisoma tena Zaburi 119:11 inasema''moyoni mwangu nimeliweka neno lako nisije nkakutenda dhambi'' Daudi alijua kuwa neno la Mungu likikaa ndani yake si rahisi kwake kuanguka dhambini. ukisona mstari wa 9 inatuambia kuwa ni kwa jinsi gani kijana atasafisha njia yake.......ni kwa kufuata na kutii neno lake. Kwaiyo utalitiije neno la Mungu kama usomi? Kwaiyo bado tunaona umuhimu wa neno yaan Mungu katika maisha ya ushindi.
       Katika waefeso 6:16-17 inasema'' ipokeeni chepeo ya wokovu na upanga ambao ni neno la Mungu''. Sasa unahitaji nini tena maana vita vyetu si juu ya damu na nyama, kwaiyo kumbe kama skari vitani ukiwa na neno your fully equiped yaan kama ni bunduki unayo, magwanda umevaa, begi la kubebea vitu unalo, mabuti unayo, upanga unao n.k...... Ukisoma Joshua 1:8 uataona kwa anasisitiza kuwa na neno na kulitafakari ila nimefurahishwa anaposema '' Ndipo utakapostawi na kufanikisha njia yako.
       Wapendwa wengi wetu hatuna biblia ambayo ndo silaha ya mkristo na bado wengine tunazo biblia lakini ni jumapili kwa jumapili yaani namaanisha unaisoma jumapili kanisani tena ni kufatisha tu yale asemayo Mchungaji ila baada ya pale ni hadi jumapili ijayo aukama kuna ibada siku za katikati. sasa tunategemea vipi kushinda???? sawa maombi ni silaha ila bila neno ni bure ni sawasawa na mtu ana bunduki ila haina risasi alafu yuko mstari wa mbele vitani!!!!! pata picha nini kitatokea.
       Uko mfano wa watu fulani ambao walikua wanafunga ndoa yao. sasa wakati watu wanatoa zawadi, wengine wakatoa gari, friji, dressing table n.k. ila kuna jamaa mmoja yeye aliwazawadia Biblia, tena aliomba kwa mc na akaongea kuwa hana chochote ila kwa kuwatia moyo maharusi wale wakasome( akataja sura na kitabu wakasome). Maharusi walipofika nyumbani wakaiweka Biblia juu ya kabati na kuisahau. siku moja mama alipokua anasafisha kabati akaikuta na kuikung'uta maana ilikua na vumbi mno. alipokua ana kung'uta akakumbuka ile sura aliyowaambia yule jamaa wakaisome, la haula! si akakuta cheque........yule mama alifurai na kurukaruka , akamwita mumewe pia, mumewe alivyokuja walifurai sana.....baada ya furaha kupungua, jamaa si akaisoma vizuri! oooouuuuhh!!! kumbe tarehe ilikua ishapita. cheque ya milioni kumi!  Huo ni mfano tu kwa jinsi gani hawa watu hawakuona umuhimu wa Biblia.


BE BLESSED YOU ALL......( stay inspired)
   
      
         

Friday, November 27, 2015

SOMO: KWANINI VIJANA WANASHINDWA KUISHI MAISHA MATAKATIFU?

Bwana yesu asifiwe wapendwa, natumai hamjambo na mu wazima wa afya.......Dhumuni la somo hili ni kujua ni kwa sababu gani tuna shindwa kuishi maisha matakatifu.
Kwanza kabisa namshukuru mungu kwa kunipa mafunuo juu ya somo hili, kwa sababu imekua kazi kwa sisi vijana kuishi maisha yanayompendeza mungu. sisemi kwamba mimi naishi maisha matakatifu kwa asilimia mia...hapana!!!! wote tunajitaidi katika fuufikia ukamilifu aliousema bwana yesu kuwa na tuwe wakamilifu kama yeye(MUNGU) alivyo mkamilifu math 5:48......ila wapo ambao ni wakristo lakini imekua historia kwa wao kuishi maisha ya utakatifu yaan kwa maana nyingine ni wakristo jina tu.
UTANGULIZI.
Kwanza kama kijana tambua yafuatayo ili uweze kushinda;
1. KIJANA NI MWENYE NGUVU(kimwili na kiroho)
mithali 20:29 '' fhari ya vijana ni nguvu zao''. 1 yoh 1:14b ''nimewaandikia vijana kwa sababu mna nguvu....'' Kwaiyo hapa tunaona dhairi ya kuwa vijana ni wenye nguvu hata biblia imethibitisha hilo...sasa shetani anajua hilo pia kwaiyo hana mda wakuangaika na wababa au wamama wakati vijana ambao ndio taifa la kesho mpo. anajua thamani uliyonayo kwa ajili ya kanisa na taifa lako na ndo maana anakutafuta usiku na mchana.
2. UJANA NDIO MSINGI WA MAISHA(wakati muhimu)
kipindi cha ujana ndio wakati sahihi wa wewe kufanya maamiuzi(future plans) za maisha. muhubiri 12:1'' mkumbuke muumba wako siku za ujana...kabla hazijaja zile mbaya'' maombolezo 3:27'' ni vyema mwanadamu achukue nira wakati wa ujana''. kwaiyo, bado tunaona shetani anatambua hilo pi na ndo maana anataka akuvuruge kipindi hiki ili usiwe na future nzuri. yohana 21:18'' wakati wa ujana ulikua ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako lakini utakapo kua mzee utainyosha mikono yako na mwingine atakufunga na kukupeleka usikotaka''
sasa tuangalie kwanini tunashindwa kuishi maisha matakatifu.....
1. KUISHI KTK MWILI... warumi 8:13-14''mkiishi kwa kuyafuata mambo ya mwili mwataka kufa bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa roho, mtaishi.....wengi tunashinda kwasababu tunaishi mwilini, atuwezi kushinda bila roho mtakatifu kukaa ndani..
1tim 2:22, math 26:41b''roho i radhi ila mwili udhaifu'' kwaiyo roho inawezekana inataka ila mwili wako bado ni kikwazo..kumbuka paulo alisema nilipendalo silifanyi ila nisilolipenda nalifanya. gal 6:8, efe 4:22-24'' inatuambia mvaeni roho mtakatifu......kwaiyo bila shaka tukimvaa roho sidhani kama habari itakua ni ya kushindwa tu....na hili ndo tatizo kuu kishi mwilini.
2. KUJICHANGANYA
1yoh 2:15,17 tatizo lingine la sisi vijana ni kuipenda dunia.....mstari huu unasema'' msiipende dunia na mambo yaliyomo ndani yake'' sasa unatakaje kuishi maisha matakatifu wakati hutaki kuachana na dunia? ukisha okoka umekua adui wa dunia soma 1yoh 3:13'' msistaajabu ulimwengu ukiwachukia''.
3.MARAFIKI/ MAHUSIANO
sababu nyingine ni marafiki tunaochagua. mara nyingi nasema na imeshawai kunitokea, uchaguzi wa marafiki au mahusiano ulio nayo wanachangia sana katika ushawihi. uwezi ukasimama wakati unaambatana na wasio amini. 2wakorinto 6:14'' usifungwe nira pamoja na wasio amini''. mithali 13:20, 1korinto 15:33, 15:11..........
MBARIKIWE WOTE KWA KUSOMA..........surely something will change after reading this......shalom!!!!!
for more information 0715918940

SOMO: UNAITUMIAJE NEEMA ULIONAYO?

Bwana yesu asifiwe friends, ni matumaini yangu mu wazima wa afya. ni siku nyingine tena ambayo bwana ametuwezesha kuiona. napenda kukushirikisha somo jingine ambalo bwana amenipa.
UTANGULIZI:
Kwanza tuanze kwa kuangalia neema ni nini? katika tafsiri ya kamusi ya kisasa inasema, neema ni mafanikio alionayo mtu kutokana na majaliwa ya mwenyezi mungu au juhudi zake, baraka n.k. kwa tafsiri yangu, Neema ni nafasi ya upendeleo au kuchaguliwa bila kustahili.
Wengi tunafikiri kuwa imetoketokea tu tupo hai hadi sasa hivi, si mgonjwa, si kilema, huna matatizo alafu unajisifu ukidhani wewe unafaa sana mbele za Mungu. kama tulivyoona hapo juu, umependelewa au umechaguliwa bila kustahili.
Hivi fikiria kwa mfano leo Mungu akakutokea alafu aseme anataka kukuchukua pumzi yake au la umpe mabilioni ya pesa!!!! nani angeweza?????.....kwaiyo bado ukijaribu kutafakari unaona kwamba umepewa nafasi(CHANCE) bila kustahili.
ukisoma yakobo 4:6 inasema'' mungu huwapinga wajikuzao bali huwapa neema wanyenyekevu.
waefeso 2:8-9, paulo anasema''kwa maana nimeokolewa kwa neema kwa njia ya imani ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu ni kipawa cha Mungu wala si kwa matendo mtu yeyote asije akajisifu.....heri yake paulo alijua kwamba kuishi kwetu ni neema yake mungu...Wapo watu wanaojisifu. jamani tambueni kuwa umepewa neema na Mungu wala si kwa mapenzi yako ila ni kwa makusudi yake...Nimetoa mfano hapo juu, kwamba kama Mungu angesema tumlipe kwa pumzi yuliyonayo, basi dunia ingekua haina mtu.2wakorinto 1:12, 6:1''Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure....
SASA UNAITUMIAJE NEEMA ULIYONAYO?
tuangalie tena 1Wakorinto 15:10''Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyokuwa kwangu si bure bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote wala si mimi bali ni neema ya Mungu pamoja nami.... Hapa tunaona paulo anasema kwa sababu hivo alivyo ni kwa neema ya mungu basi alizidi sana kufanya kazi kupita wote. Kwaiyo baada ya kutambua kuwa umepewa neema, ni vyema sasa ukaishi katika mapenzi yake kwelikweli maana mda wowote atataka umrudishie pumzi yake.
2Timotheo 2:1''Basi wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu...Anaposema tuwe hodari maana yake ni tufanye kazi ya mungu kwelikweli hali tukijua kuwa neema tuliyonayo hatukustahili. Pia kuitumia vizuri neema yetu ni kuzidi kutenda mema na kuwa watakatifu maishani mwetu.(SISI NI WASAFIRI DUNIANI)
somo hili mungu alinipa kwa makusudi yake na ni naamini kuwa wakristo tuliowengi bado hatujajua kuwa tunaishi kwa neema na neema hiyo tumepewa kwa kusudi lake....Kuna wengine tunaishi maisha ya uvugu uvugu, hatutaki kuwa committed na kazi ya Bwana. Endelea tu kufanya dhambi, maana hata biblia inasema mwenye dhambi na azidi kufanya dhambi na mtakatifu na azidi kujitakasa...sasa wewe utajua ufanyeje maana mtu mzima alazimishwi ila anachuja kabla ajafanja.ni ombi langu kuwa kuanzia leo, ebu tuanze kuitumia neema hii ipasavyo, Mungu anatuangalia tu na kutupima,kuna siku atachukua neema yake na ndipo utajuta kuwa kwa nini uliichezea...soma zaburi103:8-9 anasema''bwana amejaa huruma na neema, haoni huruma upesi, ni mwingi wa fadhili. Kwaiyo Mungu anatuvumilia tu ila ataposema sasa yatosha, Ndugu hakika utajuta.pia ukisoma warumi 2:4-5 inasema'' au waudharau wingi wa wema wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta uapate kutubu... mstari wa tano unasema kwa ugumu wa moyo wako wajiwekea hakiba ya hasira ya mungu katika siku ile ya hukumu.
kwaiyo Ndugu zangu tutumie hii neema vizuri ingali tuliwa hai....
MUNGU AWABARIKI SANAAA!!!!!!
unaweza kunipata pia katika facebook kwa mafundisho zaidi.
shalom!!!!!!!!