SHALOM!! Namshukuru Mungu sana sana kwa wingi wa fadhili na neema zake kwetu, hakuna mtu ambae alistahili kuiona siku ya leo. juzi nilikua naangalia taarifa kuna jamaa kakatwa mapanga na kufa palepale, jiulize we ni nani au umempa Mungu nini kwa uhai ulionao? kristmas imepita tunatazamia kuuona mwaka mpya..ambayo ni wiki ijayo tu ila tuendelee kumsihi Mungu atuvushe kwa ushindi.
Leo ntawashirikisha somo kama linavyosomeka hapo juu.....inawezekana ukajiuliza huyu Yesu tunamvaaje? Wengi wetu tuna lundo la nguo ambazo tunavaa na kubadilisha kila siku hakuna anae penda kuvaa nguo ileile siku zote hata kama hana ila anatamani siku awenazo nyingi. sasa ninaposema tuvue miili yetu na tumvae Yesu namaanisha kuacha mambo yakale na kuishi maisha mapya. Nimetoa mfano wa nguo maana ni kitu ambagho kinavaliwa kila siku ila sasa tofauti inakuja kwamba tukishamvaa Yesu, yeye anakua ni vazi la kudumu tofauti na nguo za kawaida hakuna haja ya kuvumvua tena.
Tuangalie katika Waefeso 4:22-24 anasema " Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu ktk haki na utakatifu wa kweli. maandiko tuliyosoma hapo juu yako wazi sana. kwaiyo tunapofanywa upya, tunapotubu na kuishi maisha matakatifu, tunapookoka ina maana tunavua miili yetu na kumvaa Yesu. wengi wetu leo bado wanang'ang'ania miili yao ya zamani wakati washampokea Yesu kristo. ndugu ni ngumu kushinda dhambi kama tunaishi katika mwili. sasa tumapo mva Yesu ni rahisi sana maana yeye ndo anatushindia yote.
Rum 8:13 inasema "kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. kwaiyo bado tunazidi kuona kwamba miili yetu haiwezi kustahimili dhambi bali tuyafisha mambo ya mwili kwa Roho ambayo ndo sawa na kusema kumvaa Yesu hakika tutaweza.
Pia tukiangalia katika Wagalatia 5:16 inasema" basi enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. neno hapa linasema mwili hunashindana na Roho, kumbuka Yesu alisema katika mathayo kwamba Roho i radhi ila mwili u dhaifu......kwaiyo kwa kumvaa Yesu na kuvua miili yetu ndo kuenenda pamoja na Roho ambae ndo anatusaidia kuweza. sura ya 6:8 anasema " maana yeye apandaye kwa mwili atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. 3:27 inasema "maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo, mmemvaa Kristo. pia Paulo anasema sura ya 2:20 " nimesulubiwa pamoja na Kristo,laakini ni hai, wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu.
Paulo anaendelea katika wafilipi 1:21 anasema" kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Kwaiyo wapenzi katika somo hili tunaona kuwa tukiishi katika miili hii pasipo msaada wa Roho ni vigumu kumpendeza Mungu, na huo msaada wa roho unakujaje ni pale tunapo mvaa Yesu kama maandiko yanavyosema
.
Tukiwa tunaelekea mwaka mpya, ni maombi yangu kuwa tuanze sasa na Bwana, tusahau yaliopita ya mwaka 2015.....anasema katika neno lake ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya. kama tumvaa yesu kikwelikweli hakika mwaka 2016 kwako unaenda kuwa wa mafanikio na baraka tele, yale ulioomba mda mrefu yatatimia kwa jna la Yesu!!!!!
Tuangalie katika Waefeso 4:22-24 anasema " Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu. mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu ktk haki na utakatifu wa kweli. maandiko tuliyosoma hapo juu yako wazi sana. kwaiyo tunapofanywa upya, tunapotubu na kuishi maisha matakatifu, tunapookoka ina maana tunavua miili yetu na kumvaa Yesu. wengi wetu leo bado wanang'ang'ania miili yao ya zamani wakati washampokea Yesu kristo. ndugu ni ngumu kushinda dhambi kama tunaishi katika mwili. sasa tumapo mva Yesu ni rahisi sana maana yeye ndo anatushindia yote.
Rum 8:13 inasema "kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. kwaiyo bado tunazidi kuona kwamba miili yetu haiwezi kustahimili dhambi bali tuyafisha mambo ya mwili kwa Roho ambayo ndo sawa na kusema kumvaa Yesu hakika tutaweza.
Pia tukiangalia katika Wagalatia 5:16 inasema" basi enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili. kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka. neno hapa linasema mwili hunashindana na Roho, kumbuka Yesu alisema katika mathayo kwamba Roho i radhi ila mwili u dhaifu......kwaiyo kwa kumvaa Yesu na kuvua miili yetu ndo kuenenda pamoja na Roho ambae ndo anatusaidia kuweza. sura ya 6:8 anasema " maana yeye apandaye kwa mwili atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. 3:27 inasema "maana ninyi nyote mliobatizwa katika Kristo, mmemvaa Kristo. pia Paulo anasema sura ya 2:20 " nimesulubiwa pamoja na Kristo,laakini ni hai, wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu.
Paulo anaendelea katika wafilipi 1:21 anasema" kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
Kwaiyo wapenzi katika somo hili tunaona kuwa tukiishi katika miili hii pasipo msaada wa Roho ni vigumu kumpendeza Mungu, na huo msaada wa roho unakujaje ni pale tunapo mvaa Yesu kama maandiko yanavyosema
.
Tukiwa tunaelekea mwaka mpya, ni maombi yangu kuwa tuanze sasa na Bwana, tusahau yaliopita ya mwaka 2015.....anasema katika neno lake ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya. kama tumvaa yesu kikwelikweli hakika mwaka 2016 kwako unaenda kuwa wa mafanikio na baraka tele, yale ulioomba mda mrefu yatatimia kwa jna la Yesu!!!!!
Anza 2016 na maisha mapya na hakika utamwona Bwana..........................................
STAY INSIPIRED!!!!!!!!!!!!!!!
STAY INSIPIRED!!!!!!!!!!!!!!!