Friday, January 22, 2016

SOMO: BADILIKA ILI UBADILISHE WENGINE.


Bwana asifiwe watu wa Mungu!
badiliko maana yake hali inayokuweko baada ya kutokea mageuzo fulani........
Katika somo hili, kubadilika kwa watu kunatokana na maisha yetu kwa asilimia kubwa sana,tunapowashuudia watu tunatamani waachane na dhambi kisha waokoke na kuja makanisani mwetu...lakini tunasahau kwamba inawezekana sisi tukawa ndio chanzo cha wao kutokuokok, mfano wewe labda una rafiki yako hajaokoka, na we umeokoka na unaishi maisha yanayompendeza Mungu, unapomshuudia habari za yesu ni rahisi kwake kubadilika maana anacho kiona ndani yako na unachosema vina uhusiano. ila pata picha wote mnazitungua dhambi kama kawaida alafu unamwambia abadilike, atabaki anakushangaa tu!
Mdo 13:47 inasema "kwasababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, nimekuweka uwe nuru ya mataifa upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia. Tafkari maneno haya kwa umakini mkubwa sana. Mungu anasema ametuweka tuwe nuru kwa mataifa ina maana kile tufanyacho kiwe chanzo cha mabadiliko kwa wasiomjua Mungu. ndio maana ya kuwa nuru yaani matendo yetu mema yawaangaazie mataifa ili kufikia wokovu ndio maana anamalizia na kusema "upate kuwa woovu hata mwisho wa dunia. hapo juu nimesema tunatamani sana kuona watu wanaokoka na pengine tunashuudiaga mitaani mwetu ila tunasahau kwamba maisha yetu yana impact(matokeo) kwa wasiomjua Mungu.kama we ni muhuni usishangae wao kuwa wahuni. lazima uwe kielelezo ili yule unayemshuudia avutike.
Tito 2:6-7 inasema " vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na kiasi 7 katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na astahivu. mfano mimi ninaye wafundisha haya kila siku lazima kwanza niwe kielelezo kwenu nyie ili kusudi muamini kile nisemacho. ni mgumu kumwambia mtu abadilike wakati wewe hujabadilika. hapa Paulo alikua anamwambia Tito kuwa awaonye vijana lakini kama hiyo haitoshi yeye kwanza awe mfano kwao.
Isaya 46:6 inasema" naam asema hivi ni neno dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kuziinua kabila za yakobo na kuwarejeza watu waisraeli waliohifadhiwa, zaidi ya hayo ntakutoa uwe nuru ya mataifa upate kuwa wokovu wangu hata mwisho wa dunia.
Luka 2:32 inasema" nuru ya kuwa mwangaza wa mataifa na kuwa utukufu wa watu wako waisraeli. bado anasisitiza kuwa nuru ya mataifa lakini kama nilivyosema huwezi nuru wakati we ni giza! mfano tube light ni nyeupe na ukiwasha mwanga unakuwa mweupe kadhalika kwa zile za bluu, njano na mwanga wake unakuwa hivyohivyo. sasa pata picha ikiwa nyeusi.......................
mwenye masikio na asikie Roho asema na kanisa...AMINA
STAY INSPIRED!!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment