Tuesday, January 5, 2016

SOMO: TAMBUA VIZUIZI VYA MAENDELEO.


Bwana Yesu apewe sifa....leo ntaenda kufndisha juu ya somo la kutambua vizuizi vya maendeleo yako binafsi.
Kama Mkristo, upaswi kuwa maskini kabisa maana katika Mithali 8:18 anasema utajiri na heshima ziko kwangu, naam utajiri udunuo na haki. Zaburi 24:1 inchi na vyote viujazavyo ni mali ya Bwana. yako maandiko mengi yanayoonesha kuwa mtu wa Mungu hutakiwi kuwa maskini kabisa maana nijuavyo mimi Mungu ni Baba yetu na sisi kama watoto ni warithi wake.....sasa haiwezekani na kamwe haitotokea eti Baba ni tajiri alafu mtoto ni maskini........uliona wap? Mfano ikitokea baba yako amekua milionea, pengine hata kusoma unaweza ukaacha maana unajua hata iweje huwezi kulala njaa, kukosa maitaji n.k.
sasa zipo sababu kwanini watu wa Mungu hatufanikiwi. kama somo linavyo someka hapo juu, kuna vitu vinazuia maendeleo yako Mtu wa Mungu....sa nyingine sio kwamba umevamiwa na pepo hapana! sikatai kuna maroho ya umaskini na ufukara yanayofuatilia watu wa Mungu ila kuna vitu ni vya kuchukua hatua tu na mafanikio yatakuja. haleluyah!
1.KUTOKUA NA MALENGO(nia)
Ni wachache sana wanaofanya vitu kwa kuweka nia na malengo juu ya hivyo vitu. wapo watu anasoma lakini hajui hata anasoma ili iweje au anataka kuwa nani hapo badae. watu we dont have FOCUS on the things ahead. leo tunashuudia watu ndoa zinawashinda kwa sababu wanashindwa kumudu gharama za maisha, ni kwasababu hapo awali walikua wakiishi tu bila kujali mbele yake itakuaje mwishowe wanakurupuka kwa sababu kila mtu anaoa basi naye anatimiza wajibu.....mfano mzuri ni katika mpira, wanaopenda watakubaliana na mimi...unajua kwa nini nchi za wenzetu ziko juu na zinafanikiwa? ni malengo na nia waliojiwekea toka awali. waliandaa vijana ambao sasa hivi ndo wanatisha..angalia Tanzania, sio kwamba tuna pepo la hasha! hatuna mipango ya badae kila kukicha wanataka Timu iamke asubuhi moja tu alfu ghafla wajikute wako kombe la dunia.(jiulize kuwa kina samatta na ulimwengu kwanini wanafanikiwa)
kutokua na malengo ni kama mtu anaejenga nyumba bila kuwa na ramani...sijawai kuona na sijui hiyo nyumba itakuaje! Luka 14:28 inasema maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama kwamba anavyo vya kumalizia?. Yesu alitoa mfano huu ukiwa ni dhairi kuwa unatakiwa kuwa na lengo au nia ya kufanya kitu.
2.UVIVU/KUPENDA USINGIZI
unakuta tu mtu mvivu anapenda kulala balaa alafu huyohuyo mtu analalamika hana mafanikio anaomba maombi. nakwambia tutamuombea hadi nywele zitanyonyoka! Mithali 6:9-10 ewe mvivu utalala hata lini?utaondoka lini katika usingizi wako? sura ya 13:4 nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu. 10:4 atendaye mambo kwa mkono wa mlegevu huwa maskini. bali mkono wake aliye na bidii hujitajirisha. 20:13 usipende usingizi usije ukawa maskini fumbua macho yako nawe utashiba chakula.
Biblia imesema sana juu ya watu wavivu, kupenda usingizi. kwaiyo mwenye bidii lazima afanikiwe.siku tafuta muda wako nenda kwa matajiri unao wajua watakwambia, lazima walikua na bidii. ndio kuna watu wanatajirika kwa urithi ila bado kuna bidii atafanya kumantain utajiri ule awezi kukaa tu. sasa niambie hapo kama unaitaji maombi wakati we ni mvivu na unapenda usingizi? kama we si mvivu na umefanya kila liwezekanalo alafu hali ni ileile, hapo sasa maombi yanaitajika.
MAWAZO HASI(NEGATIVE THOUGHTS)
ninaposema negative thoughts yaani mtu badala ya kuwaza mambo ya kimaendeleo, anawaza kumsema mtu, kulipiza kisasi,anawaza anasa tu, na vitu vingine vingi.Mithali 21:5 mawazo ya mwenye bidii huelekea utajiri tu, bali kila mwenye pupa huelekea huitaji. hili linaendana na hapo juu, mtu mvivu awezi waza maendeleo ye ni kuwaza ale kwa mpendwa gani kwa siku hiyo, hawezi waza kufanya kazi. 28:19 alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele bali afuataye mambo ya upuuzi atapata umaskini wa kumtosha. napapenda hapa maana amesema vizuri sana. yaani afuataye mabo ya upuuzi ina maana upuuzi anao uwaza kama nilivyosema hapo juu.kwaiyo like uwazacho kina impact kubwa sana katika maisha yako ukiwaza upuuzi basi ndivyo utakavyo kuwa ukiwaza maendeleo utayapata maana ndicho uwazacho mfano mtu anawaza kufelifeli tu katika masomo yake ni lazima atakua wa kufeli maana akishawaza moyoni mwake na mentality yake sasa inakua hivyo hivyo na mwisho wa siku hata kusoma inakua shida.......
3.KUTOKUA NA (STS)
STS ni
-SELF DISCIPLINE(nidhamu binafsi)
-TIMEMAHAGEMENT(kukomboa wakati)
-SAVING(kujiwekea akiba)
niliona kuwa vitu hivi vina humimu mkubwa sana katika kuleta maendeleo yako binafsi. wengi wetu leo hatuna nidhamu binafsi, hatukomboi wakati, na hatujiwekei akiba.
TIME MANAGEMENT(kukomboa wakati)
waefeso 5:15-16 basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu waio na hekima bali kama watu wenye hekima. mkiukomboa wakati kwa maana zama hizi ni za uovu. Kol 4:5 enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
kwaiyo wakati ni jambo moja la msingi sana. kuna msemo sa hivi mtu anasema eti naenda beach kupetezapoteza muda! aisee kama ulikua unasema hivyo acha kabisa, time is not to be wasted!
unapopangilia mda wako unaokoa vingi sana.......Watanzania swala la mda linatugalimu coz tumeka waswahili sana hatutunzi muda. we angalia kwa mfano we mwenywe shuleni ukipangilia time table yako binafsi ya kujisomea kuifuata ni shida.
SELF DISPLINE(nidhamu binafsi)
nidhamu binafsi ni kuwa na utaratibu mzuri wa kuendesha maisha yako. kuna msemo unasema usipo jiheshimu uwezi kuheshimiwa.
2 Thes 3:11 maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu hawana shuguli zao wenyewe lakini wanajishugulisha na mambo ya wengine. kwaiyo how do you expect a person like that awe na maendeleo? mtu hana utaratibu wa kujiendesha hajui afanye nini ni ngumu kufanikiwa.
SAVING( akiba)
ni wangapi leo tuna tabia ya kujiwekea akiba? neno la Mungu linasema Mithali 6:8 lakini hujiwekea akiba ya chakula watati wa jua hukusanya chakula chake wakati wa mavuno. ukijizoeza kuweka akiba sasa hivi uwezi kupata tatizo hapo badae maana vipo vya kutosha. sa hv unakuta watu wanaishiwa kupita maelezo na ndio maana kukopana kumezidi. mi mwenyewe ni lisumbuka sana na hili tatizo paka pale nilipogundua. akiba ni jambo muhimu sana wapendwa!
STAY INSPIRED!!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment