Friday, January 29, 2016

SOMO: USIFICHE UTHAMANI ULIONAO.

 SOMO: USIFICHE UTHAMANI ULIONAO.
Bwana apewe sifa.......
Kwanza nataka kila mtu atambue kuwa wewe ni wathamani, ukisoma 2Wakorintho 6:20 inasema "maana mlinunuliwa kwa thamani " anaposema mlinunuliwa kwa thamani, ndugu nataka ujue kuwa ulipookoka ilikuwa ni kitendo cha wewe kununuliwa na Mungu,tena kwa thamani kama alivyotangulia kusema hapo juu.
Kwanza nataka kila mtu atambue kuwa yeye ni wathamani, ukisoma 2Wakorintho 6:20 inasema "maana mlinunuliwa kwa thamani " anaposema mlinunuliwa kwa thamani, ndugu nataka ujue kuwa ulipookoka ilikuwa ni kitendo cha wewe kununuliwa na Mungu, tena kwa thamani kama alivyotangulia kusema hapo juu.
Thamani maana yake ni gharama au ubora wa kitu kutokana na hali na kuhitajika kwake kwa jamii. kwaiyo anavyosema, mlinunuliwa kwa thamani maana yake tuna ubora na tunahitajika kwa jamii inayotuzunguka. Sasa wapo wanaoficha uthamani wao nikiwa na maana ya kwamba wapo ambao wanaogopa kutambulika kama wameokoka. pengine mtu anaogopa labda atachekwa na wenzake, atatengwa na jamii, au wakijua atashindwa kuwa huru maana anataka kuendelea na dhambi. Ndigu tambua kuwa Mungu amekuweka uwe nuru ya mataifa kwaiyo unapojificha ni sawa na kuwasha taa alafu ukaifunika au ukaiweka chini ya pishi.
Matendo 4:13 inasema" basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa, wakastaajabu wakatambua kuwa walikuwa pamoja na Yesu. Nimeapenda pale anaposema hawakuwa na elimu ila watu walistaajabu maana Roho Mtakatifu aliwapa elimu ya kutosha. Hapa tunaona ujasiri wa Petro na Yohana, wenzetu hawakuona tabu ya wao kuhubiri injili na hata kuwa tayari kufa kwa ajili ya Kristo. Rum 1:16 inasema" kwa maana siionei haya injili kwa sababu ni uweza wa Mungu uletao wokovu.kwaiyo unona ni jinsi gani walikuwa wantambua. sasa hivi imekuwa ni shida hata kwa mkristo kwenda kushuudia maana hana ujasiri kwasababu atachoenda kuwakataza wenzake ndicho afanyacho.
2Tim 2:12 inasema" kama tukistahimili tutamiliki pamoja naye, kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi. mfano mzuri ukisoma Mathayo 26:69-79 utaona jinsi petro alivyo mkana Yesu mara tatu, ila ana heri maana iliomba msamaha palepale! unaweza ukawa umemkana yesu tayari, unaokuwa chuoni kwako, maeneo ya nyumbani na hutaki watu wajue umeokoka,huakondiko kumkana, katika Mathayo, Petro akutaka ajulikane kwasababu aliogopa kufa pamoja na Bwana wake! pengine na wewe leo unaogopa kujulikana kwa sababu rafiki zako watakukimbia, au jamii inayokuzunguka itakutenga........SIKIA! ukisoma Luka 9:26 inasema "kwa sababu kila atakaye nionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa Malaika watakatifu. 12:9 inasema "na mwenye kunikana mbele ya watu huyo atakanwa mbele ya Malaika wa Mungu. uunapoona haya kwa sababu nilizotaja hapo juu, tambua hiyo ndiyo haya atakayo kuonea Yesu kristo mbele za Mungu. katika Mathayo 10:32 inasema"basi, kila mtu atakayenikiri mbele za watu, nami nitamkiri mbele za baba yangu. kwaiyo ndugu zangu, tubadilike, aiwezekani tunataka watu waokoke, waje kwa Yesu wakati sisi hatutaki kubadilika.......dont expect changes to others kama wewe mwenyewe ujabadilika.
STAY INSPIRED!!!!!!

No comments:

Post a Comment