Tuesday, January 12, 2016

SOMO: TUMECHAGULIWA ILI TUFANYIKE WANA WA PENDO LAKE.


Shalooom! hope everybody's fine na mwaendelea vizuri...sifa na utukufu ni kwake
Leo tutaenda kujifunza somo kama linavyosomeka hapo juu. Nataka utambue kuwa tumechaguliwa kwa kusudi maalumu na ndio maana nilkalipa somo langu kichwa cha habari kwamba tumechaguliwa ili tufanyike wana wa pendo lake.
KWANINI TUMECHAGULIWA?? kabla ya kumpokea yesu naamini tulishuudiwa ama tulisikia habari za kuokoka na ndipo labda ulipochukua hatua, sasa kile kitendo cha kuchukua hatua yaani kuokoka ndio kuchaguliwa kwenyewe!! angalia Yohana 1:12 inasema " bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu ndio wale waliaminio jina lake......Biblia ya kingereza tafsiri ya NIV inasema"he gave them the right to be become children" tunaona kuwa ukisha okoka moja kwa moja tayari unakuwa ni mwana wa Mungu.
1 Yohana 3:1 inasema " tazameni pendo la namna gani alilotupa Baba kwamba tuitwe wana wa Mungu na ndivyo tulivyo. tunaona makusudi ya Mungu kutuokoa. anaposema pendo alilotupa Baba kwamba tuitwe Wana wa Mungu ni kwamba alituokoa ili tuingie katika ufalme wake yaani tuwe wana wake. kama mtu wa Mungu unatakiwa kutambua kuwa umetengwa au umechaguiwa. kitendo cha kuokoka ni kuchaguliwa yaani imediately unapokua umeokoka jina lako linafutwa katika kitabu cha kuzimu na kuandikwa katika kitabu cha uzima, huko ndo kuchaguliwa!
Wakolosai 1:13 inasema "naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katia ufalme wa Mwana wa pendo lake. embu tafakari maneno haya;
hatua ya kwanza aliyoifanya Mungu ni kutuokoa, wengi tulikua dhambini, watumwa wa dunia kwaiyo alichokifanya Mungu ni kukutoa katika nguvu za giza na kukuleta kwake na ndio maana kwa mfano tunapowashuudia watu ili waokoke au mtu anapookoka anakua amevutwa na Mungu kutoka kwenye nguvu za giza.
hatua ya pili akatuamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake. unaweza ukajiuliza kwanini nimesema kuna hatua ambazo Mungu alifanya! lengo au kusudi la Mungu kutuokoa ni kutuingiza katika ufalme wake kwaiyo yeye akiisha kutuokoa kazi ya pili ni juhudi zetu ni kuhakikisha kwamba tunateka ufalme wa Mungu..sikia, Mathayo 11:12 inasema" Tangu siku za yohana mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu nao wenye nguvu wauteka. kwa mstari huu nadhani utakua umeelewa kwamba iko kazi ya ziada kuuteka ufalme wa Mungu.
Sasa tuangalie kwa karibu hii hatua ya pili.2 Wakorinto 6:17 inasema "tokeni kati yao mkatengwe nao, asema Bwana, msiguse kilicho kichafu, nami nitawakaribisha. kama nilivyosema Baada ya hatua ya pili ambayo ni kukuhamisha na kutuingiza katika ufalme wake, 2 Wakorinto 6:17 inatuambia cha kufanya sasa hili tuuteke au tuingie katika ufalme wake. kile kipengele cha mwisho anasema nami ntawakaribisha, sasa atatukaribisha wapi??? ina maana ndio atatukaribisha katika huo ufalme. na ni baada ya kupambana kama tulivyosoma katika Mathayo 11:12.
Usifikiri kwamba tukiisha okolewa moja kwa moja ni Raha tu hapana!! iko gharama sasa ambayo ndo inatupeleka katika ufalme wake.
Warumi 8:29 inasema" maana wale aliowachagua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndigu wengi. kwaiyo tatizo linakuja au unaweza ukajiuliza kama Mungu alituchagua kwanini tunashindwa na ibilisi???? Mpendwa, watu wengi wanashindwa kutambua kuwa ukisha okoka umechaguliwa kwaiyo hakuna kurudi ulipotoka ndio narudi katika ile hatua ya pili ya kuuteka ufalme wake....sasa usipoelewa kuwa umechaguliwa kwa makusudi , huwezi au ni ngumu kusonga mbele. mfano ni pale labda mwanafunzi anapochaguliwa kujiunga na sekondari, au labda umefaulu form 4 ukachaguliwa....ukishaenda shule uliochaguliwa si jukumu tena la necta au wizara ya elimu iliyokuchagua kuja kukusomea ili ufaulu au likupitishe tena katika hatua ifuatayo..hapana! ni juhudi zako.
STAY INSPIRED!!!

No comments:

Post a Comment