Saturday, January 16, 2016

SOMO: TAFUTA KUMPENDEZA MUNGU NA SI MWANADAMU.


Praise the living God.........! inawezekana kweli umeokoka, uko vizuri kiimani lakini ukawa unampendeza mwanadamu badala ya Mungu wako.....fuatilia mtiririko huu utaelewa.
katika Wagalatia1:10 " maana, sasa je! ni mwanadamu ninao washawishi, au Mungu? au nataka kuwapendeza wanadamu? kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
haya ni maneno ya Paulo kwa wagalatia. unaweza ukaona ni kwa jinsi gani mtume Paulo alitambua kazi aifanyayo ni kumpendeza Mungu na si mwanadamu. wengi wetu leo tunawapendeza wanadamu wenzetu na si Mungu. mfano wapo watu ambao wanaenda kanisani kwa kuhofia kwamba mchungaji atamuuliza au mshirika mwenzake atamuuliza. yaani ile dhamira yake ya kufanya kazi ya Mungu haitoki moyoni bali anafanya ili aonekane machoni pa watu tu!
kuna ule mfano niliutoa wa rafiki yangu alieogopa kuja kanisani kuokoka ili nikunirishisha. mi nasema ana heri yule jamaa maana anatambua ya kwamba haifaidii kitu mimi kufurai kwa kuwa ntaona kuwa amebadilika lakini moyoni mwake ni tofauti. ndio maisha ya wakristo wengi siku za leo, anaendaa kanisani ili baba yake au mama yake afurai tu au ili mshirika mwenzake afuraishwe pia. na kuna wanaogopa kuwa wataulizwa maswali na mchungaji wao. si washirika tu, wapo wachungaji wanao wanyenyekea washirika kwa mfano unakuta kuna msirika anatoa sana katika ujenzi, michango, anamsaidia labda kusomesha watoto wa mchungaji, anamtegemeza sana mchungaji n.k sasa unakuta mchungaji anaaza kumnyekekea kiasi cha kwamba hata yule mshirika akikosea ni ngumu kwa mchungaji kumwadhibu. mwisho wa siku yule mchungaji anaanza kuweka hofu kwa mshirika wake badala ya Mungu. sababu kubwa ya watu kuwapendeza wanadamu pengine ni kutomjua Mungu vizuri.
1 Thess 2:4 inasema" bali kama vile tulivyopata kibali kwa Mungu tuwekewe amana injili, ndivyo tunenavyo si kama wapendezao wanadamu bali wampendezao Mungu anayetupima mioyo yetu"( amana ni kitu anachopewa mtu na mtu mwingine ili amtunzie au amwekee, akiba, kitu cha thamani kubwa) Paulo anajaribu kutueleza tena kuwa tumpendeze Mungu anaetupima mioyo yetu. kumpendeza mwanadamu kuna mwisho wake ni sawasawa mtu anaye mtegemea mwanadamu labda watoto walikua wanamtegemea baba sasa amefariki pata picha shida watakayo ipata wale watoto.
Mathayo 6:1 inasema" angalieni msifanye wema machoni pa watu kusudi mtazamwe na wao kwa maan mkifanya kama hayo hampati thawabu kwa baba yenu aliye mbinguni. mstari huu ananifurahisha sana maana anasema hampati thawabu mbele za Mungu. pale juu nilitangulia kusema kwamba inawezekana umeokoka vizuri na ukajua unaenda mbinguni ila bado kikwazo kikawa ndio hiki cha kumpendeza mwanadamu. Yesu aliwaambia waangalie au unaweza sema kwa lugha nyingine jihadharini msije mkafanya wema machoni pa watu. na ndivyo ilivyo leo kwamba mtu anataka asifike kuwa alitoa kiaisi kadhaa kanisani kwenye mchango wa ujenzi ila dhamira yake siyo tumtolea Mungu bali apate sifa kuwa anazo! utasikia mi nimefanya hiki, nimefanya kile kwa kanisa langu tena niliweka bati lote peke yangu, au mtu anasaidia yatima, wajane, wenye shida ili watu wauone wema wake kumbuka kuwa huko ndiko kumpendeza mwanadamu na si Mungu.
mstari wa23:5 inasema" tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu kwa kuwa hupanua hirizi zao huongeza matavua yao. yaani yote hii ni kwamba mtu anafanya ili aonekane tu......na watu wa leo walivyo huwa wanasubiri watu wote wawepo ili aonekane kabisa wala hawezi fanya pekeyake pekeyake.
Kwaiyo wapendwa embu tutafute kumpendeza Mungu, tufike seheme na sisi tuwe kama mtume Paulo aliyetambua kuwa kazi yake si ya kumpendeza mwanadamu.....BARIKIWA!
STAY INSPIRED!!!!!!!

No comments:

Post a Comment