Sunday, January 3, 2016

SOMO: JIFUNZE KUACHILIA ILI MUNGU AKUSAMEHE.


Watu wengi atujui maana ya kusamehe na kuachilia. katika kichwa cha habari hapo juu nimetumia neno kuachilia, maana unaweza ukasamehe na usiachilie.inawezekana ushawai kusikia ule msemo kwamba nimekusamehe ila sito kusahau. Mungu anataka tuachilie sio kusamehe peke yake. kuachilia ni kusamehe na kutokumbuka kamwe.
Hivi pata picha kama Mungu asinge kusamehe wewe ungekua wapi? sasa swali linakuja unashindwaje kusamsamehe mwenzako?? Mungu ni zaidi ya mzazi kwetu,kuna wengi leo wamefukuza na wazazi wao au pengine wamekorofishana na hawapatani hadi leo sababu labda kuna kosa mmoja wao alimfanyia mwenzake. ila kwa Mungu hali ni tofauti, unazidi kumuudhi kila kukicha lakini yeye ana kusamehe tu. jana ulikua unaiba na leo uko kanisani, yeye anasamehe, unajifanya umeokoka ila una mambo yako ya chinichini, yeye anasamehe tu.
swali langu ni kama Mungu anakusamehe na kusahau yale uliofanya jana, mbona tunashindwa kuwasamehe waliotukosea?
Wengi tunaijua sala ya Baba yetu na pengine tumeiimba sana tukiwa sunday school ya watoto na pengine hata leo tunazidi kuziimba. ukisoma Math 6:9 anasema Baba yetu ulie mbinguni jina lako litukuzwe.............................................................................................sasa, ukiendelea mstari wa 12 unasema utusamehe deni zetu kama na sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu!!! hebu jaribu kutafakari,nikweli unachosema? au kwasababu ni sala na imeandikwa katika Biblia basi unasema tu? Maana yake hapo unamwambia Mungu akusamehe wewe kwasababu juzi na wewe uliwasamehe waliokukosea. sasa swali linakuja Mbona wewe hukusamehe sasa kwanini unataka wewe usamehewe? Ni ngumu watumishi si kama tunavyodhani....Luka 17:3-4 anasema jilindeni ndugu yako akikosa mwonye, akitubu msamehe. na kama akikukosa mara saba ktk siku moja na kurudi kwako mara saba akisema nimetubu, msamehe. sikia hapo juu Yesu alisema hata akikukosa mara saba, Petro aliambiwa samehe saba mara sabini, of coz hakuna mtu akosae kiasi hicho kwa siku lakini Yesu alikua anajaribu kuonesha kuwa no matter makosa yanayofanywa na watu kila siku kwako, wewe samehe tu. kwaiyo yesu alivyosema saba mara sabini that means ni 470.....sasa nani anaweza kufanya hivyo ingawa kosa moja tu ulilofanyiwa mwaka jana na ndugu yako umelishikilia moyoni mwako hutaki hata kumwona!!!!
Marko 11:25 nanyi kila msimamapo na kusali, sameheni mkiwa neno juu ya mtu, ili Baba yenu alie mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.26 lakini kama ninyi hamsamehe wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu. nimependa aliposema kuwa sameheni ili na Baba awasamehe na ninyi makosa yenu. kwaiyo unaweza kuona kuwa unaposamehe Mungu nae anakusame makosa yako. sa nyingine tumekuwa hatujibiwi maombi yetu maana tunamwendea Mungu wakati mioyo yetu imebeba machungu na machukio juu ya watu, hapo juu amesema msimamapo na kusali. kwaiyo kumbe kutokusamehe inaweza ikawa chanzo cha kutojibiwa maombi. unaweza ukamkuta mtu anavyotubu mbele za Mungu analia na kuomboleza huku akimbembeleza Mungu amsamehe, neno liko wazi samehe usamehewe basi yaani fomula ya Mungu ni ndogo sana.
Math 5:7 heri wenye rehema maana hao watapata rehema.
kuna wapendwa wansema wameokoka na mbinguni wanaenda ila ukiwakuta hata kanisani hawaongei ni chuki kwa kwenda mbele...sasa sijui ni mbingu ipi hiyo ya watu wa namna hiyo. kwanza ni jambo la ajabu hivi inakuaje unachuki na mpendwa mwenzako? na mataifa watafanyaje? Kanisa la leo upendo hakuna, Umoja hakuna...watu wanahama makanisa eti kisa mpendwa mwenzake kamkwaza! mambo mengine sio ya kukemea, unakuta mtu anaomba Mungu amsaidie asiwe na hasira alafu kesho na keshokutwa mtu akikukwaza una kasirika. badae unaenda kwa mchungaji akuombee, uwezi pona. hilo swala ni lakucontrol wala si kuomba. chukua hatua ujicontrol alafu katika kujicontrol kwako ndipo umuombe Mungu akusaidie.
4give everything that happened last year and the past years....this year is going to be a prosperous year for you,only if you 4give and start a new page in your life!!!!
STAY INSPIRED..!!!!!

No comments:

Post a Comment