Thursday, January 14, 2016

SOMO: MSIMAMO WAKO KWA MUNGU UKO WAPI?


Yesu asifiwe wapendwa....
Labda kwa kuanza, tuangalie nini maana ya msimamo. katika kamusi ya sasa inasema msimamo ni mawazo ya mtu yenye kuonesha mtazamo wake kuhusu jambo au tendo la kufuata kanuni fulani za maisha.
Baada ya kuona nini maana ya msimamo, pengine tutakua tumeshajua msimamo ni nini!
Msimamo kwa kingereza unaweza ukasema principles.....i believe everyone of us have his or her own principles in life, kama huna thats a shame na tambua unaishi ili mradi maisha yaende tu. Msimamo ni kitu kimoja cha muhimu sana katika maisha, mfano katika mahusiano wengi wetu wanapenda kujua principles za wenzi wao. sasa kwanini msimamo?? msimamo unakusaidia kujiendesha kimaisha. mtu anaejiendesha bila msimamo ni rahisi sana kufanya makosa au kutofanikiwa. mfano kwa wadada ambao wanatongozwa tongozwa ovyo na wakaka, kama hana msimamo wake binafsi ni rahisi kumkubali kila mtu alafu mwisho wa siku kujilaumu.....au kwa mfanya biashara kama hakuna msimamo wa nini ufanye ili ufanikiwe unaweza ukashawishiwa na wenzako na kujikuta kila siku unabadilisha biashara na hakuna mafanikio.
Sasa nikienda kwa upande wa kiroho, kama kichwa cha habari kinavyosema, wengi wetu hatuna msimamo na ndio maana inakuwa rahisi sana kwa mwamini kuanguka au kurudi nyuma.yakitokea mabaya tena yuko tayari hata kumkana yesu kama petro... ili tu asipate tabu au asidhurike. tena wengine wakienda mikoani ndio huwezi tambua hata kama wameokoka. anakuwa kinyonga ghafla!!
kuna pasta fulani alikua na kanisa kubwa tu...hakupendezwa sana na waumini wake maana walikuwa hawapo serious na ibada mara leo waje kesho wasije. siku pasta akamwalika pasta mwenzake ila akamuomba kuwa akija aje kama gaidi,avamie kanisa na kuua wale wanaompenda Mungu.
ilipofika jumapili, wakati ibada inaendelea mara yule pasta akavamia kanisa mkononi akiwa na bunduki.....watu waliogopa sana! yule pasta alisema wote wanaompenda Mungu wasogee mbele huku mikono ikiwa juu, alivyomaliza kukoki bunduki tu, hakukua na mtu kanisani kasoro pasta, wote walikimbia.
huo ni mfano wa kwamba watu wale hawakua na msimamo juu ya Mungu wanae mwabudu. je ingetokea leo ungebaki?????
Danieli 1:1-30, mstari ni mingi sana sitaiandika ila naomba ukasome na uone jinsi watu hawa wa Mungu walivyokua na msimamo mbele za Mungu. wote tunaijua hii stor vizuri sana ila naomba ukasme kwa umakini sana. nawapenda hawa watu sana maana ukisoma mstari wa 16 inasema" ndipo shadracka meshaki na abednego wakajibu wakamwambia mfalme, ee nebukadreza hamna haja kukujibu katika neno hili 17, kama ni hivyo Mungu wetu tunaemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto naye atatuokoa na mkono wako. 18, bali kama si hivyo ujue ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
hivi embu tafakari maneno ya hawa watu wa Mungu alafu jiulize mimi na wewe tungeweza kweli???? yaani hawa jamaa walikuwa tayari kwa lolote lile ambalo lingekuja mbele yao. labda nikufumbue macho unapokuwa na msimamo mbele za Mungu yeye akuachi. angalia mstari wa 24, ndipo nebukadreza akastaajabu akainuka kwa haraka akanena akawaambia mawaziri wake je! hatukutupa watu watatu hali wamefungwa katikati ya moto? wakajibu wakamwambia, mfalme kweli.
Mungu awezi kukuacha uaibike kamwe! Msimamo wa watumishi hawa ulibadili hata utaratibu wa nchi...kitu cha ajabu sana!
Ni rahisi sana kwa wapendwa kusema wameokoka na wanampenda Yesu lakini hawana misimamo mbele za Mungu. Petro alimwambia Yesu kuwa yuko tayari hata kufa nae ila badae baada ya petro kuona shuhuli ni nzito alimkana mara tatu ila heri yake yeye ambaye alitubu palepale.
msimamo unakusaidia kuishi maisha yanayompendeza Mungu...................
STAY INSPIRED!!!!

No comments:

Post a Comment