Tuesday, January 19, 2016

SOMO: UTAMWENDEA YESU KWA MASHAKA HATA LINI?


Bwana yesu apewe sifa....natumai mu wazima wa afya.
shaka ni nini? hali ya kujawa na wasiwasi na kukosa uhakika wa jambo. hiyo ndo maana ya shaka yaani una kuwa na wasiwasi, huna uwakika na kile ufanyacho.
wengi leo tunamwendea Yesu wetu kwa mashaka na ndio maana hatufanikiwi, hatujibiwi maombi kwa sababu hatuna uwakika na kile tunachokiomba tumejawa wasawasi. pengine unayo imani ndio lakini ni ndogo. ukisoma biblia ya kingereza tafsiri ya NIV inasema" you with little faith"!
Math 18:22-31 Yesu aliwaambia wanafunzi wake wavuke watangulie ng'ambo, huku yeye akibaki kuomba. wakati wanafunzi wamefika katikati, kukkawa na dhoruba kali. ndipo Yesu aliwaendea akienda kwa migu juu ya bahari. wanafunzi walipomwona akitembea juu ya maji wakadhani ni kivuli wakaingiwa na hofu. sasa point yangu inakuja mstari wa 28 "Petro akamjibu akisema Bwana ikiwa ni wewe niamuru nije kwako juu ya maji 29, akasema njoo, Petro akashuka chomboni akaenda kwa miguu juu ya maji ili kumwendea yesu 30, lakini alipouona upepo akaogopa akaanza kuzama! akapiga yowe akisema Bwana niokoe. Mara Yesu akaunyosha mkono wake akamshika, akamwambia ewe mwenye imani haba mbona uliona shaka?
Unaona Petro alipouona upepo aliogopa akaanza kuzaama. kwaiyo alipoogopa tu ndipo alipoanza kuzama ina maana Yesu alivyomwita hakuzama bali alianza kuzama pale alipoona shaka.
Thats how things are today pipo! inawezekana vitu vyako haviendi sawa, haufanikiwi, umeomba lakini hakuna majibu, tambua ya kwamba ulifanya kwa mashaka. Petro alianza kuzama alipoona shaka. alitamani na ndio maana akamuomba Yesu ili nayeye atembee juu ya maji lakini alipoona shaka biblia inasema akaanza kuzama. Yesu yuko tayari kukusaidia ila tatizo unaona shaka!
Yakobo 1:6 inasema " ila na aombe kwa imani pasipo shaka yoyote, maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari linalochukuliwa na upepo na kupeperushwa huku na huku." angalia mtu mwenye shaka alivyofananiswa hapa, anasema ni kama wimbi la bahari linalochukuliwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Mungu anataka tuwe na imaani tumuombapo. Yohana inasema nanyi mkiomba lolote kwa jina langu aminini kwamba yatakuwa yenu. hakusema kwamba msubiri yatakuwa yenu hapana! anasema amini tu.
unajua kuna muda huwa nawashangaa watu, wanaona kama miujiza haiwezekani sikatai kuwa kuna watu wana fuataga nguvu za uponyaji nigeria.......ila kwa udogo wa imani yako inafika kipindi huamini kabisa miujiza. tusome Marko 11:23 inasema" amini nawaambia yeyote atakayeuambia mlima(pepo) huu ng'oka ukatupwe baharini wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia yatakuwa yake. sasa unataka nini tena hapo wakati maandiko yako wazi kwamba unao uwezo wa kuamisha milima yaani kukemea pepo na zikatoka ila amesisitiza kuwa usione shaka!
kwaiyo saa nyingine tatizo liko kwako mwenyewe kumbuka pale juu tuliona tatizo lilikuwa la petro maana alianza vizuri ila kwa sababu aliona shaka moyoni mwake ndio maana alimaliza vibaya. vivyo hivyo na wewe yamkini unamwendea yesu kwa mashaka kama petro, na ndio maana tatizo ulilo nalo limekuwa sugu, unataka uponyaji ila una mashaka, wasisi unahisi kama Mungu awezi kukuponya. kumbuka yule mama alietokwa na damu miaka kumi na miwili laiti kama angeona shaka wakati anagusa pindo la vazi la Yesu yamkini hadi leo angekuwa anataabika na ugomjwa wake ila kwa kuwa aliamini toka moyoni, basi pindo tu liliweza kumponya........
STAY INSPIRED!!!!!!!

No comments:

Post a Comment