Sunday, January 10, 2016

SOMO: DHAMBI NI KIKWAZO CHA UPONYAJI.


Shaloom!!!!
katika somo hili, nimegundua kuwa dhambi imekua chanzo cha mambo kuharibika ktk maisha yako hususani maisha ya mwamini! ila leo ntaongelea jinisi gani dhambi imekua kikwazo cha uponyaji.....( SI UPONYAJI WA MWILI TU HATA WA KIROHO)
1 KIROHO
katika Yakobo 5:16 inasema "ungamaneni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana mpate kuponywa" jiulize swali kwamba kwa nini Mungu alisema muombeane ili mponywe ila kabla ya kuponywa, ameanza kwa kusema ungamaneni? Kama kuna kitu Mungu anachukia ulimwenguni basi ni dhambi. kuna sehemu kwenye biblia inasema "dhambi ni chukizo kwa Mungu" Mungu anachukia sana dhambi, ukisoma katika Mwanzo 6:5-6 inasema " Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila analowaza moyoni mwake baya tu siku zote. Bwana akaghairi kuwa amemfanya mwanadamu duniani akahuzunika moyo. yaani embu jaribu kufikiria hadi Mungu anajuta kwa nini alituumba! unaweza ukapata picha ni kwa kiasi gani anachukia maovu. sasa nilifundisha juu ya somo la kwanini unajidanganya mwenyewe? yaani unakuwa mnafiki mbele za Mungu, dhambi unaitaka, Mungu unampenda! vinaendana kwa karibu. unaposhilikilia dhambi ni ngumu kwako mpendwa kuponywa roho yako. inapofikia kipindi unaona uko vibaya kiroho na unahitaji uponyaji, kama bado hutaki kuacha maovu, tambua ya kwamba ni vigumu sana kupokea uponyaji wako.
Isaya 66:2b inasema" lakini mtu huyu ndiye ntakaye mwangalia mtu alie myonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu. Mungu anamwangalia mtu mnyenyekevu, dhami ufanyazo zinamzuia Mungu kutenda kitu katika maisha yako ya kiroho. mfano, mvuta bangi ameokoka anakuja kanisani kama kawaida tena vizuri ila akitoka anarudi vijiweni kwake anaendelea na bangi kama kawaida........mtu huyu hata ataombeje ili aache tatizo la kuvuta bangi itakua ngumu sana maana kwanza yeye mwenyewe bado anayoshauku ya kuendelea na hiyo dhambi hivyo ni ngumu kwa Roho mtakatifu kumsaidia maana hataki kusaidika ingawa anaomba.
2 Nyakati 7:14 inasema "ikiwa watu wangu walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe yao na kuiponya nchi yao......kwaiyo bado andiko hili linatudhihirishia kuwa dhambi ni kikwazo cha uponyaji. hapa Mungu anasema nitaiponya nchi ila kabla ya kuponya anataka tuache njia mbaya kwa maana ya toba.
2 KIMWILI
swala la pili hapa ni uponyaji wa kimwili yaani magonjwa yanayowasumbua watu. yupo mdada mmoja aliokoka mkutanoni kanisani kwetu ila alikua na mapepo yaliomsumbua mda mrefu sana kiasi cha kumpa magonjwa. tuliomba na kuomba paka! funa siku tulipokua tunaomba tuliwauliza yale mapepo kwanini hawataki kuondoka ndipo walitujibu kuwa ana vitu vyao na ndio maana hawataki kwenda.....tulipovichoma moto yule dada alifunguliwa palepale!
Mungu anapata kikwazo kukuponya maana umeishikilia dhambi nabado hutaki kuiacha. mapepo hawaoni sababu ya kukuacha wakati bado unajenga mazingira ya kukaa nao.
Zaburi 103:3 inasema " akusamehe maovu yako yote, akuponya magonjwa yako yote" tunazidi kuona kuwa kabla ya kukuponya magonjwa yako kinachoanza ni kusamehewa kwanza. Mungu awezi kukusamehe na dhambi zako hata siku moja. ni either utubu na upate uponyaji au uendelee na dhambi na kuteseka katika magonjwa.
katika Mthayo 9:1-3 tunaona kuwa walipomleta yule mwenye kupooza akiwa kitandani, Yesu alisema "jipe moyo mkuu mwanangu, umesamehewa dhambi zako" Yesu alimsamehe dhambi zake kwamza aliharuhusu uponyaji maana kama nilivyosema hapo juu, dhambi ni kikwazo cha uponyaji. somaa popote pale hasa katika vitabu vya injili, Yesu alikua ana ponya na kumwambia huyo mtu kuwa asitende dhambi tena au anasamehe dhambi ili kuruhusu uponyaji ndani yake.
Kwaiyo mpendwa, dhambi ni kikwazo cha uponyaji wa kimwili na kiroho pia. dhambi imekua chanzo cha kutobarikiwa pia na kupata mafanikio katika maisha yetu.....
STAY INSPIRED!!!!!!!!

No comments:

Post a Comment