Saturday, January 2, 2016

SOMO: WEWE NI WA THAMANI MBELE ZA MUNGU.


Bwana asifiwe, ni furaha ilioje kuuona mwaka. Tunamshukuru Mungu kwa kweli maana ni wengi walitamani. kwa mwaka huu wa 2016, nimeona niendelee na mtiririko wangu wa masomo na leo ntaenda kufundisha juu ya uthamani wako kama mkristo hasa kijana ulieokoka.
UTANGULIZI
Mtu ukishaokoka lazima utambue kuwa wewe ni wa thamani mbele za Mungu. Mungu anatuona kama wa thamani sana mbele zake na ndio maana alisema atakae kugusa anagusa mboni yake! kwaiyo unaweza pata picha juu ya thamani ulionayo mbele za Mungu. 
USIHARIBU UJANA WAKO.
Vijana wengi tunapoteza thamani yetu mbele za Mungu kwa kuharibu ujana wetu.
1. ZINAA, hivi ushawai kukaa na kufikiri kwamba unaharibu usichana au uwanaume wako? kwa mfano mtu ukiwa na mchumba ukazini ane akakuacha, akaja mwingine ukazini nae, mwingine na mwingine...pata picha kama utakua na utofauti na anae ujiuza kama ni tofauti ni kwamba yeye hana watu maalumu ila wewe unao basi hiyo ndio tofauti. 1Thes 4:4 inasema kila mmoja wenu na ajue kuuweka mwili wake katika utakatifu. 1Kor 6:18 inasema ikimbieni zinaakila dhambi aitendayo mwanadamuni ne ya mwili wake ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake, ukiendelea mstari 20 inasema maana mlinunuliwa kwa thamani. sasa basi mtukuzeni Mungu katika miili yenu. so kitu kikubwa hapa ni zinaa. vijana wengi leo wanashindwa kujizuia na shetani kwakua anajua huu ni udhaifu wa vijana kwa kweli anakesha usiku na mchana akihakikisha anadhoofisha vijana. nilikutana na mtu akasema kwamba kwa kweli yeye asipo zini kuna kitu kinapungua ndani yake na anahisi atakufa. nataka nikuhakikishie kwamba zinaa inazuilika na wala hautakufa, zinaa sio chakula kwamba usipokula utakufa au utadhoofika LA HASHA! sio kwamba nasema haya tu, mimi mwenyewe nilidhani hivyo ila baada ya kukombolewa hakika naanza kujuta kwa nini nilikua nazini kabla ya wakati wa ndoa.
nakumbuka kuna rafiki yangu aliniambia kua ukizini jua kua unaharibu maisha ya mke wa mtu ajae.....mithali 6:32 inasema mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa, afanya jambo linalomwangamiza nafsi yake. wimbo ulio bora 3:5 enyi binti za yerusalemu msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha hata yatakapoona vyema yenyewe.
KWANINI ZINAA?
I)TAMAA ZA MWILINI, Mithali 6:25 inasema usitamani uzuri wake moyoni mwako usikubali akunase kwa kope za macho yake.1Tim 2:22 inasema zikimbieni tamaa za ujanani ukafuate haki. 1Petro 2:11 inasema wapenzi nawasihi kama wapitai ziepukeni tamaa za mwilini zipinganazo na roho. Kwaiyo hapa tunaona chanzo kubwa la kuanguka katika dhambi ya zinaa ni tamaa ya mwilini....unaweza ukasema mbona nashindwa kuicontrol? angalia Rum 8:13. sababu ni kuishi katika mwili, laiti kama tukiyafisha mambo ya mwili kwa Roho Mtakatifu hakika utaweza.
ii) MAMBO YA DUNIA, usitegemee kuwa utashinda majaribu ukiwa bado unaipenda dunia..1Yoh 2:15 msiipende dunia wala mambo yaliyomo katika dunia. mithali kama nilivyosema uwezi ukashinda majaribu wakati unayapenda, unakuta kijana ameokoka vizuri tu lakini hana tofauti na ambao bado hawajaokoka kwanini? ni kwa sababu yale alioyashikilia bado, yanaendelea kumzonga zonga mfano umeokoka lakini bado disko unataka kwenda, bar unaendelea ila kwa kisingizio unakunywa soda tu, bado manyimbo ya dunia unayo tena kwenye simu yako...labda nikufumbue., nyimbo hizo hazina utukufu na kila kinachoimbwa katika nyimbo hizo kuna maroho kama nyimbo ni mapenzi basi roho ya mapenzi haiwezi ikakuacha ng'o!
iii) marafiki/mahusiano, wengi wamepotea hasa kwenye sehemu hii. 1:10 mwanangu, wenye dhambi wakikushawishi wewe usikubali. 2Wak 6:14 msifungwe nira pamoja na wasioamini kwa jinsi ilivyo sawasawa kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? tena panashirika gani kati ya nuru na giza? mithali 24:1 usiwahusudu watu waovu wala usitamani kuwa pamoja nao. kwaiyo marafiki wana ushawishi mkubwa sana kwako kama ulikua hujui. yaani kama rafiki yako hataki kuacha dhambi kwa vyovyote ukishirikiana nae lazima nawwe utashawishika tu. mithali 13:30 inasema enenda pamoja na wenye hekima uatakuwa na hekima. hivyo hivyo ukienenda na wafanyao dhambi nawe utakua mtenda dhambi. ukisoma Mwanzo 34:1 utaona jinsi dina alivyo shawishika na marafiki zake atakuvunja usichana wake maana alikua hamjui mwanaume.
AINA ZA UPENDO
nataka kuongelea aina za upendo maana viana wengi tunakosea sana tukidhani tunapendwa kumbe sio.
1.UPENDO WA TAMAA, upendo huu ndo umekua sababu kubwa sana ya watu kuumia na kuumizwa katika mahusiano.....hapo juu nimeongelea tamaa, upendo wa tamaa unaanzia machoni na si moyoni n baada ya macho kuona unawasiliana na mwili wako ndipo unapohisi kuwa umependa kumbe umetamani. mfano mkaka anaweza kumwona mdada barabarani akamfata na kumwambia kuwa na kupenda...hapo dada unatakiwa kujua hiyo ni tamaa upendo wa kweli si wa ghafla.....1Samweli 13:1 tunaona jinsi amnoni alivyompenda dada yake tamari. ule haukua upendo wa kweli ulikua ni tamaa na ndio maana ukisoma mstari wa 15 amnoni akamchukia machukio makuu sana. mkaka akishakupenda, ukikubali akishazini na wewe kama ilikua tamaa lazima atakuacha tu maana hicho ndicho kilicho msukuma kwako. na ndio maana nawashauri wa dada ukiona uko na mtu na anakulazimisha mzini kataa tena mkimbie, maana upendo wa kweli huvumilia.
2.UPENDO WA HISIA, Unaweza ukashangaa lakini kuna upendo wa hisia. huu unakuja pale unapomwona mtu na kudhani unampenda ila huna uwakika. yaani unakua unahisi unampenda ila uwakika huna...sasa ushauri wangu hapa ni kwamba ukihisi kua unampenda mtu usikurupuke paka pale utakapokua na uwakika maana inawezekana ikawa no mwanzo wa kuharibu future yako. mfano kama ni mdada ukahhisi unampenda mkaka na ukamwambia inawezekana huyo kaka yeye akupendi na mwisho wa siku mabo ni yaleyale ya amnoni na tamari........atakuchezea na kukuacha.
3.UPENDO WA KWELI,huu unaanzia moyoni ukiangalia 1Petro 3:4 anasema na kuwe na utu moyoni usioonekana, ktk mapambo yasiyo haribika yaani roho ya upole na utulivu iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 1kor 13:1-13 yaani mimi naupenda sana maana characheristics za true love ziko hapa. mstari wa 4upendo huvumilia, hufadhili, hautakabari, haujivuni, haukosi kuwa na adabu, haufuati mambo yake. unajua ni tatizo letu tu sisi vijana lakini unaweza ukaomba na Mungu akakupa mtu sahihi wa maisha yako sasa tatizo linakuja tunaomba wakati tupo kwene mahusiano tayari.

No comments:

Post a Comment